JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MALIASILI NA UTALII
Your browser may not support display of this image.

TAARIFA KWA UMMA
KUMILIKI KISHERIA WANYAMAPORI AU MASALIA YA WANYAMAPORI

Wizara ya Maliasili na Utalii inatoa taarifa kuwa mtu yeyote haruhusiwi kumiliki nyara za serikali, yaani mnyamapori au kipande chochote cha mnyamapori, bila kibali kutoka kwa Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori. Hii inatokana na Kifungu cha 86(1) na (2) cha Sheria ya Kuhifadhi Wanyamapori Sura Na. 283 ya mwaka 2009 ambacho kinapiga marufuku kumiliki nyara kinyume cha sheria.

Kwa mfano, mtu yeyote haruhusiwi kumiliki, chui, simba, punda milia, fisi, au mnyama yeyote kwa sababu yoyote ile bila kibali kinachotolewa kisheria.

Sheria ya Kuhifadhi Wanyamapori Sura Na. 283 inatoa tafsiri ya nyara za serikali kuwa ni mnyamapori aliye hai au aliyekufa ikiwa ni pamoja na masalia yake. Masalia hayo ni kwa mfano pembe, mifupa, ngozi, kucha, kwato, nyama, nywele, manyoya, mayai, au sehemu yoyote ya mnyamapori au nyara zilizotengenezwa.

Wizara inawataka watu wote wanaomiliki nyara bila vibali watoe taarifa na maelezo kuhusu namna walivyopata nyara hizo kwenye Ofisi za Idara za Wanyamapori za: Wilaya,Mkoa, Mapori ya Akiba au Kikosi dhidi ya Ujangili. Baada ya uhakiki taarifa hizo zitawasilishwa Idara ya Wanyamapori Makao Makuu ili uamuzi sahihufanyike kuhusu kuhalalisha umiliki huo au vinginevyo.

Kutokana na Kifungu cha 87(1) cha Sheria ya Kuhifadhi Wanyamapori Sura ya 283 Wizara inamtaka mtu yeyote atakayeona nyara za serikali zikimilikiwa na mtu asiyehusika, au asiyekuwa na kibali, kutoa taarifa kwa kwenye ofisi za Maliasili, Wanyamapori au Polisi.

Kwa maelezo zaidi wasiliana na:-

Mkurugenzi,
Idara ya Wanyamapori
S. L. P 9372
Dar es Salaam
Simu: 0754 833229 au 0754  292008 au 0754 695766  Email: dw@mnrt.go.tz
{MWISHO}
George Matiko
MSEMAJI
WIZARA YA MALIASILI NA UTALII
7 Aprili 2012

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. Sungura naruhusiwa kumiliki? au na yeye mpaka kibali?

    ReplyDelete
  2. na hao wanyama mnauza nje ya nchi kila siku inakuwaje??

    ReplyDelete
  3. je waweza kutofautisha mfupa wa swala na mbuzi? au mtafanya DNA test

    ReplyDelete
  4. Kucha na Pembe za wanyama! - Duh! - Naona Serikali imeanza kuwaandama Waganga wa Kienyeji pamoja na Wachawi! - maana wao ndio huwa wanatumia kucha na mapembe kwenye shughuli zao

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...