Mwana Libeneke Mkongwe nchini Haki Ngowi na Edna Kyando wamemeremeta leo katika kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es salaam na kuhitimisha siku yao kuu kwa mnuso wa nguvu katika hoteli ya Golden Tulip.
Timu nzima ya Michuzi Media Group inayoendesha libeneke la Globu ya Jamii inatoa pongezi kwa mwana libeneke mwenzetu Haki Ngowi na mai waifu wake Edna Kyando kwa kumeremeta leo. Tunawatakia maisha mema, ya furaha na fanaka. Libeneke Oye!

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 7 mpaka sasa

  1. ah!Hongereni sana Mungu awabariki,
    kumbe mzee haki ngowi ulikua bado upo upo tu? hivi wale ffu walivyoimba haki ngowi ughaibuni ana libene lake,
    ndo kusema libeneke lenyewe ndio hivyo

    ReplyDelete
  2. kweli ffu walivyoimba "Msione milango na Madarisha" "Majumbani mnafichwa mambo" kumbe mzee ulikua hupo hupo tu?

    ReplyDelete
  3. Hongera Bwashee,hongera Edna..Karibu kwenye bahari yetu hii yenye mawimbi ya kila aina.Mimi na mai wafu wangu tuna miaka kumi tunaogelea..Ni balaa..Sasa mnaweza kuvua hayo maboya yenu,ila mimi nawashauri mvae maboya yenu muda wote wa safari kwa sababu kunaweza kutokea mawimbi mazito wakati wowote.Kila la kheri.........

    Davod V

    ReplyDelete
  4. edna mdogo wangu umependeza mno, upendeze hivyo hivyo miaka yote, wish you the very best.
    dadio, naila

    ReplyDelete
  5. Wacheni kebehi kuhusu watu kuchelewa ktk suala la Ndoa!

    Mkae mkijua kuwa Dunia ya sasa ina changamoto na masuala kama ndoa ni mazito sana na ndio maana watu huwagharimu ktk kuchaguana kutokana na wengi wetu kuyachukulia maisha kuwa kitu rahisi kama maigizo ya Mchezo wa Runinga!

    UNAWEZA KUWA NA PUPA NA HARAKA KTK NDOA UKAJIKUTA UMEUVAA MKENGE, UKALIINGIA GALACHA UKAKWAMA KIMAISHA AU UKAFA HARAKA KULIKO VILIVYO TENA NDANI YA KIPINDI CHA MAFANIKIO YAKO KIMAISHA BAADA YA KUSOTA KWA MUDA MREFU UKITAFUTA MAISHA!

    ReplyDelete
  6. Congrats Mzee HakiNgowi, nakutakia kila la kheir kwenye maisha yenu ya ndoa. Mungu awatangulie

    Rafikiyo, Sele wa Kijichi

    ReplyDelete
  7. AnonymousMay 04, 2012

    hongereni saana Edna n Haki ngowi mmependeza saaaana kiukweli bi harusi ana natural beauty jamani she is pritty niempenda ila ndio kawaiwa hivyooooooooo.....

    all the best

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...