Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akisalimiana na wananchi waliojitokeza kumpokea katika uwanja wa karume Pemba alipowasili kisiwani humo kwa ziara maalum kuangalia maendeleo katika sekta mbali mbali za kijamii.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la MapinduziDk.Ali Mohamed Shein,akisalimiana na Mtoto Suleiman Shaaban Juma,pamoja na wanachama wa Kampuni ya Mkipi Miliki Tungamaa,kuzindua Mradi wa uzalishaji wa sabuni kwa kutumia mashine maalum ya Mkipi Miliki,leo akiwa katika ziara kisiwani Pemba,kuangalia maendeleo ya jamii.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la MapinduziDk.Ali Mohamed Shein,akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu George M.Buchwafwe, wakati alipoangalia Sabuni iliyotengenezwa katika kampuni ya Mkipi Miliki Tungamaa,ambayo inayozalisha sabuni kwa kutumia mashine maalum,alipokuwa katika ziara ya kutembelea maendeleo katika Mkoa wa Kaskazini Pemba.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akizungumza na wananchi wa Mkipi Miliki Tungamaa, baada ya kuzindua rasmi uzalishaji wa sabuni kwa kutumia mashine maalum ya kampuni ya Mkipi Miliki,alipokuwa katika ziara ya kutembelea maendeleo katika Mkoa wa Kaskazini Pemba.
Baadhi ya watendaji wa Ofisi mbali mbali za Taasisi za serikali za Mkoa wa Kaskazini Pemba,wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la MapinduziDk.Ali Mohamed Shein,alipokuwa akizungumza na watendaji hao,wakati alipofanya ziara ya kuangalia maendeleo katika sekta mbali mbali za Mkoa wa kaskazini Pemba,katika ukumbi wa Jamhuri Hall Wete Pemba.Picha na Ramadhan Othman,Pemba.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Kaka braza Ras Makunja namuona kwa mbali!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...