Tanzania imeshinda katika michuano ya kila mwaka ya soka ya The Football4Hope-United Cup 2012 iliyodhaminiwa na SABMiller katika uwanja wa Thayagaraj Sports Complex jijini New Delhi, India. Jumla ya timu 14 zilishiriki mwaka huu, wakiwemo mabingwa wa mwaka jana, UN Organisations. Timu zingine zilikuwa Team India, Hope Team, Balozi za Denmark, China, Spain, Misri, Saudi Arabia, Indonesia, Uholanzi, Israel, Botswana na Tanzania.

Katika fainali Tanzania  waliibwaga Botswana  kwa bao 2-1.
Mechi  za awali na matokeo za Tanzania ni kama ifuatavyo:

Denmark 0-11 Tanzania
France 0-4 Tanzania
India 0-2 Tanzania
Israel 1-7 Tanzania
Hope1-5 Tanzania
--------------------------------
Spain 0-2 Tanzania
China 1-6 Tanzania
India 0-1 Tanzania
--------------------------------
Botswana 1-2 Tanzania
 Vijana wa Kitanzania wakifurahia ushindi wao kwa staili tofauti


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Hapo ni Full kizazi kipya cha taifa stars
    ikiwa taifa stars itakuwa inasaka wachezaji wenye vipaji vya ukweli kutoka sehemu mbalimbali mikoani na vijijini

    lakini kama taifa stars itaendelea kuangalia wachezaji kutoka simba yanga na azam basi tutabaki kuwa mkia duniani.

    Hongera sana vijana wetu tunajivunia kuona mnatangaza nchi yenu kwa mapenzi makubwa dunia nzima.

    ReplyDelete
  2. Hongereni kwa kupeperusha vyema bendera ya Nchin yetu..

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...