Wadau wapendwa,
Hivi tunavyoongea kuna watu wana kamchezo ka kutafuta password za email za watu na kutaka kufanya ndivyo sivyo. Wamejaribu kulamba password ya ankal bila mafanikio na sasa wanatumia email ya uwongo kujaribu kuwasiliana na wadau wangu, kama inavyoonesha juu.

 Jihadhari na ujumbe wa aina hii katika TWITTER kwani ukiwajibu tu ama ukifungua link waliyokupa, na kompyuta yako haina kinga, ujue umekwisha. Msisitizo hapa ni kwamba ukipata ujumbe wa TWITTER aina hii achana nao na badili password yako haraka sana. Hakikisha umeweka japo tarakimu moja ama mbili katika hiyo password yako. Inasaidia
- Michuzi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 08, 2012

    ankal jana nimepata DM ya twitter kwa user name yako halafu ilikua usiku wa manane..imagine nilistukaje!

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 08, 2012

    MZEE JANA USIKU NILIPOKEA MSG YAKO, NIKAHISI KUNA KITU....!! it happens hawkers pole Br Ankal - na pole pia na Bwawa letu la Maini ngoja tuone jioni hii kama tutalipiza....!! mchana mwema.

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 08, 2012

    MUSWAADA WA KATIBA MPYA:

    Inabidi tuwe na Katiba inayokwenda na wakati pia iliyo kuwa sambamba na kasi ya maendeleo ya Sayansi na Teknolojia.

    Ili tuwe na nafuu na mustakabali mzuri masuala ya namna hii yapatiwe mwelekeo ktk katiba mpya na kuingizwa kama sehemu yake.

    Kama anavyoripoti Ankali juu ya Udukuzi wa hatari aliofanyiwa!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...