Habari iliyoifikia Globu ya Jamii muda mfupi uliopita,inaeleza kuwa Mbunge wa Jimbo la Rombo kwa Tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeo (CHADEMA),Joseph Selasini (pichani) amepata ajali ya gari jioni hii katika maeneo ya Bomang'ombe wakati akitokea Arusha kuelekea Moshi.

Imefahamika kuwa Mbunge huyo amejeruhiwa huku Mama yake aliekuwemo kwenye gari hiyo akiwa amepoteza maisha.

Chanzo cha ajali hiyo bado hakijafahamika mpaka sasa,tunaendelea kufuatilia na tutapeana taarifa zaidi hapa hapa.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 7 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 25, 2012

    oooooh.....

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 25, 2012

    Poleni sana. Mungu awajalie wapone haraka.
    Bara bara zinatumaliza sasa watanzania.

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 25, 2012

    Poleni sana wanafamilia.
    Mungu awapumzishe waliotutangulia na awape afya na nguvu waliosalimika..

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 25, 2012

    Mhe Selasini poleni sana kwa lililowafika. Mama yetu apumzike katika raha ya milele. Amen. Ichube

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 25, 2012

    Na nyie magwanda hamtulii kutwa mko huku huku eh! Sasa mtasema ni magamba ndiyo wahusika?

    ReplyDelete
  6. AnonymousMay 25, 2012

    ni huzuni sana haswa ikizingatiwa walikuwa wanatoka kumzika ndugu yake mbunge ambaye ni Padre. familia imepotezana watu wawili kwa mpigo, Mola awape subira

    ReplyDelete
  7. AnonymousMay 25, 2012

    poleni sana ndugu zetu Mungu awatangulie katika muda huu Elibariki Gideon.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...