Gari aina ya Suzuki yenye nambari za usajili T 525 BWK ikiwa imeigonga bajaj yenye nambari za usajili T 581 BQY jioni ya leo na kusababisha dereva wa Bajaj hiyo kujeruhiwa.chanzo cha ajali hiyo ni kukatika kwa kamba iliyokuwa ikitumika kuivuta gari hiyo na kupelekea mtu aliekuwa anaiongoza gari hiyo iliyokuwa ikivutwa na pikipiki nyingine ya matairi matatu (haipo pichani) kushindwa kuiongoza gari hiyo na kufikia hatua hii.
 Hivi ndivyo mambo yalivyokuwa baada ya gari hiyo kuigonga bajaj
 Wasamalia wakiongea na Dereva wa Bajaj ambaye alirushwa kutoka kwenye chombo hicho hadi nje na kumfanya kujeruhiwa katika mikono yake na eneo la kichwa.
Hii ndio pikipiki yenyewe iliyokuwa ikiivuta gari hiyo.
 Mashuhuda wakiangalia tukio hilo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 28, 2012

    bongo tambarare....haahaaa!!sasa kweli hiyo kamba toka lini ikavuta gari?hapo alieumizwa hata kulipwa halipwi inakula kwake tu na samahani kibao.....

    David-Muni
    Manchester

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...