Uongozi wa Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) unafuraha kuwatangazia  kuwa huduma za safari za abiria kwenda  Kigoma zitaanzia tena Dar es Salaam  hapo Jumanne  Mei 22, 2012  badala  ya  Dodoma.
 
Itakumbukwa kuanzia Januari 24, 2012 huduma za usafiri wa abiria ilibidi zihamishiwe Dodoma baada ya eneo kati  ya Stesheni za Godegode na Gulwe  za reli ya kati ( mkoani Dodoma)  kukumbwa  na mafuriko makubwa. Hata hivyo mamlaka iliyokuwa inafanya ukarabati sehemu hiyo imeithibitishia  TRL kuwa eneo hilo sasa liko imara kwa safari za treni za abiria.

Kwa mujibu taarifa rasmi za TRL  kuanzia Jumanne ijayo usafiri  wa abiria utakuwa mara mbili kwa wiki na utakuwa katika siku za Jumanne na Ijumaa kutoka Dar es Salaam  kwenda Kigoma  ambapo treni zitaondoka saa 11 jioni. Aidha kutoka Kigoma kuja Dar safari zitakuwa kwa siku za Alhamis na Jumapili  treni itaondoka Stesheni ya Kigoma saa 12 jioni.

Taarifa imefafanua kuwa hakuna mabadiliko kwa safari ya treni ya abiria iliyopangwa kuondoka siku ya Jumapili  Mei 20, 2012 kutoka Dodoma kwenda Kigoma saa 1 usiku, isipokuwa wakati wa kurejea itasafiri moja kwa moja hadi Dar es Salaam ili kukidhi matakwa ya ratiba mpya inayoanza  Jumanne Mei 22 na Ijumaa Mei 25, 2012.

Halikadhalika Uongozi unawahimiza wananchi wanaotaka kusafiri kuanzia Dar es Salaam kwenda Kigoma wafike katika Stesheni zilizo karibu nao kwa kupata maelezo ya safari  husika na kukata tiketi wanazohitaji.

Imetolewa na Ofisi ya Uhusiano kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi Mtendaji  Mhandisi K.A.M Kisamfu
Imesainiwa na:

MIDLADJY MAEZ
MENEJA UHUSIANO- TRL
MEI 16, 2012

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 16, 2012

    Zitto Kabwe mbona suala la usafiri wa treni kutoka dar es salaam kwenda kigoma limekupita,please saidi wananchi kwenye hili pia,sio linalohusu CCM tu

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 17, 2012

    Sasa nguvu zinatakiwa zielekezwe kwenye reli, barabara zinamaliza watu. Waziri Mwakyembe rejeshea heshima reli. Kumbuka enzi za Mwalimu

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 21, 2012

    Kwa mtazamo wangu suala la reli imekuwa siasa,inamaana hicho kipande cha reli kutoka dodoma mpaka dar ndicho kichukue mwaka mzima?tunajua mawaziri wetu wanashare ktk makampuni ya usafirishaji wa mizigo sasa reli ikifanyakazi malori yao yatakosa kazi

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...