Chama Cha Mapinduzi kupitia kitengo cha Mawasiliano na Umma chini ya Idara ya Itikadi na Uenezi imeanzisha Blogu ambayo pamoja na kuhabarisha habari za mapema kabisa za shughuli za Chama, lakini itakuwa ikiyapa kipaombele pia kuhabarisha matukio mbalimbali tangu ya Kijamii, Siasa, Biashara, Uchumi, Burudani, Sanaa na Michezo na pia kupokea na kuyasambaza maoni ya wengine ili mradi yatakuwa na lengo linalotofautiana na ukiukwaji wa maadili ya vyombo vya habari.

Kwa heshima, Chama Cha Mapinduzi kinawasilisha kwako uitangaze Blogu hii kama utakavyoona inafaa, lakini pia uendelee kuanzia sasa kuwa mdau wa kuiperuzi ili kuwa chanzo chako cha kwanza cha kupata habari muhimu za kitaifa na kimataifa.

Baadhi ya dondoo muhimu kuhusiana na blogu hii zipo kwenye Logo iliyoambatanishwa na salam hizi.

Blog: CCM Chama Blog

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 10 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 07, 2012

    mbona ina mambo yale yale ya hii blog? au ni tawi lako bwana anko? hawana jipya la kuweka huko?

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 07, 2012

    Oyeeeeeeeeeee oyee oyeeee hivi ndivyo sisi wapenzi na wanachama wa hiki chama makini tunavyotaka.

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 07, 2012

    CCM ni lini mtatulia mfanye mambo yenu kisomi? Kila kitu ni kufanya kwa kukurupuka tu .. hamkai chini mkafanya kitu kwa umakini.

    Kwenye top banner/ heading mmeandika CCM Chama Blog then chini yake mmeandika www.ccmchama.blogspot.blogspot.com/ sasa hii ndio nini? Blog yenu sio hiyo mlitakiwa muandike www.ccmchama.blogspot.com. Yaani mpaka mnafikia kutangaza "public" na wala hamjaliona kosa hilo, lakini sishangai sana maana CCM ni chaka la watu sub-standard!

    ReplyDelete
  4. Che GuevaraMay 07, 2012

    Mnakumbuka shuka wakati kumekucha? kaazi kweli kweli!

    ReplyDelete
  5. MkomunistiMay 07, 2012

    najuuuta kukufahamu! Siku nyingi tulishakutoa mioyoni mwetu

    ReplyDelete
  6. CCM DAMUMay 07, 2012

    CHADEMA hoyeeeeeeeeeeeeeeeeeee!!!!

    ReplyDelete
  7. AnonymousMay 07, 2012

    Mmeiga mawazo ya NCCR-Mageuzi? maana wao wanayo siku nyingi;
    mawasilianonccr-mageuzi.blogspot.com/

    ReplyDelete
  8. AnonymousMay 07, 2012

    CHADEMA hoyeeeeeeeeeeeeeeeeee!
    sory jamani, CCM mhhhhhhhhh! hahaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!

    ReplyDelete
  9. AnonymousMay 08, 2012

    Rangi hiyo ya kijani inaumiza macho sio lazima iwe kwa wingi hivyo....

    ReplyDelete
  10. AnonymousMay 08, 2012

    SAFI SANA! PONGEZI NA HONGERA CCM. CHAMA PEKEE TANZANIA KISICHO NA UDINI, UKABILA NA UBAGUZI WA RANGI. CCM IMARA DAIMA!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...