Kwa mujibu wa Msemaji wa familia, Alex Chimila, taratibu za kuaga mwili wa marehemu zitaanza saa 4:00 asubuhi na kumalizika saa 6:00 mchana, tayari kwa msafara wa kwenda kuzika katika Makaburi ya Tegeta A, Goba, jijini Dar es Salaam.
Uamuzi wa kuaga mwili kwenye eneo hilo una lengo la kutoa nafasi kwa wadau mbalimbali kupata fursa ya kushiriki kwenye tukio hilo.
Tunawaomba waandishi wa habari za michezo na wadau wengine wa michezo na burudani kujitokeza kwa wingi asubuhi kwenda kumuaga mpendwa wetu. Rachel alikumbwa na mauti usiku wa kuamkia juzi kwenye hospitali ya Mwananyamla, Dar es Salaam.
Nawasilisha.
Amir Mhando
Katibu Mkuu TASWA
13/05/2012
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...