Hi Ankal.

Nipo na kwenye Basi la Shabiby kuelekea Dodoma,lakini mpaka sasa tupo hapa Maeneo ya Kibamba ambapo kuna ajali imetokea na kusababisha msongamano wa magari na kupelekea kuwa na line mbili mpaka tatu zote za kwenya upande mmoja (kuelekea moro).

Hivyo hakuna kupishana tena kama barabara zetu zilivyo na msongamano unazidi kuwa mkubwa,tunaomba uliwasilishe hili kwa wahusika ili waweze kulifanyika kazi haraka iwezekanavyo maana hali ni tete na hakuna askari Polisi wa usalama barabarani hata mmoja kwenye eneo hili.

Mdau J.J

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 07, 2012

    kwa nini kumekuwa na line tatu badala ya mbili. Sasa hata kunasua tutaanzia wapi. Wote waliotanua na kuifanya hiyo ya tatu niwakute mahakamani leo leo.

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 07, 2012

    Na bado itaendelea kutisha foleni za Morogoro road,Magufuli akisema ukweli anaonekana hafai hafikirii watu huyu bwana magufuri ndiye pekee atakayeweza kuondoa tatizo hili tumpe nguvu barabara haina hata njia mbadala,nyumba zimesongamana karibu na barabara hakuna hata mipango ya kuipanua hili tatizo linazidi kubwa sana na litatisha

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 07, 2012

    DAWA YAKE POLISI WAGOME NA MUACHWE HAPO HAPO. HALI HIYO HUTOKEA MARA NYINGI, WATU BADALA YA KUSUBIRI SULUHU WANAJIFANYA KUWAHI NA KUISHIA KULETA MSONGAMANO USIO NA SULUHU!

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 08, 2012

    Hapo ajali,likibomoka je??
    inakuaje kusiwe na mbadala---hili ni tz tu..niko china;wao sehemu kama hiyo wanaweka madaraja matatu na tunnel...wakijua dharula inaweza kutokea wakati wowote na mbadala unakuwepo!...leo daraja la ruvu likibomoka maisha tanzania yanasimama---mbadala wa bagamoyo baaadoo kufika kiwango

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...