![]() |
| Da' Chemi Chemponda na mwanae Elechi aliyelamba nondozzz Chuo Kikuu cha Brandeis University, Marekani |
Wadau, Da' Chemi Chemponda anafurahi kutangaza kwamba manae Elechi Henry Kadete amekula nondozzz ya Bachelor of Arts' kutoka Chuo Kikuu cha Brandeis University, Waltham, Massachusetts, Marekani. Major yake ilikuwa ni Business. Sherehe ilikuwa jumapili iliyopita. Kweli safari ilikuwa ndefu na kulikuwa na matuta mengi njiani, lakini kafika. Baba yake marehemu Prof. Henry Kadete, lazima anatabasamu kutoka mbinguni.
Brandeis ni Chuo Kikuu cha Wayahudi, lakini wanapokea wanafunzi kutoka nchi mbalimbali na dini mbalimbali. Imam alisoma sala ya kufungua sherehe. Baadaye Rabbi wa Kiyahudi, na Padre wa Kikristo walitoa sala za kufunga sherehe.
Hongera Elechi!
![]() |
| L-R Dr. Aleck Che-Mpomda (babu), Da' Chemi Chemponda, Elechi, Camara (kaka), Malaika (mama mdogo) na Mrs. Che-Mponda (bibi) Watoto wadogo ni watoto wa Malaika. Kwa picha zaidi BOFYA HAPA |




wanafanana midomo..hongera !
ReplyDeleteWow hongera sana mama na mtoto na umshukuru Mungu kwa wema alo kujalia kumtuza Elechi mpaka sasa amepata degree yake. Hongera kwa babu na bibi pia; a very touching family nimewapenda. Count yourself very lucky to have both parents at your side.bll
ReplyDeletehongereni sana, babu na bibi huwa wana uhusiano mzito sana na wajukuu zao, mara nyingine wazazi hatuwaelewi watoto wetu kama vile wazazi wetu wanavyowaelewa. Familia imeonesha upendo na umoja. Keep it up. Congrats young man God Bless you
ReplyDeleteSafi sana!Naona familia imekamilika,,,Jitahidi Elechi.Kijana,umepiga hatua kimaisha Mwenyezi Mungu Akuongoze....
ReplyDeleteAhlam UK
Hongera kwa kazi nzuri ya kulea Dada Chemi!
ReplyDeletehii ni changamoto kwa watu tusio na nondoz huku majuu. kila mwaka time kama hizi za graduations kila kona roho huwa inaniuma hope na mie iko siku nitavaa joho
ReplyDeleteHongera.
ReplyDelete