
Meli hiyo inavyoonekana kwa Nje

Meli hiyo inavyoonekana kwa ndani.

Meli hiyo inavyoonekana kwa Ujumla
---- .
Azam yaamua kufanya kweli na hivi karibuni meli ya kisasa iko mbioni kuzinduliwa ambayo ikawezesha watu kwenda na magari yao Zanzibar. Meli hiyo inauwezo kubeba magari 200, abiria 1500 na Mizigo tani 500.
KAMPUNI ya Usafiri wa baharini ya Azam Marine inatarajia kuzindua meli kubwa ya kisasa kwaajili ya abiria waendao Dar es Salaam, Pemba na Unguja. Meneja Mkuu wa kampuni hiyo Hussein Mohamed Said, amesema Julai 15 mwaka huu meli hiyo yenye urefu wa mita 100 itazinduliwa.
KAMPUNI ya Usafiri wa baharini ya Azam Marine inatarajia kuzindua meli kubwa ya kisasa kwaajili ya abiria waendao Dar es Salaam, Pemba na Unguja. Meneja Mkuu wa kampuni hiyo Hussein Mohamed Said, amesema Julai 15 mwaka huu meli hiyo yenye urefu wa mita 100 itazinduliwa.
Mohamedi alisema shida ya usafiri itapungua kwa asilimia kubwa kutokana na meli hiyo kuwa na uwezo wa kubeba abiria 1500, Mizigo tani 500 na magari 200 ambapo abiria atakae jisikia kwenda na gari lake Zanzibar, Pemba au Dar es Salaam ataweza kufanya hivyo.
Waziri Mwenye dhamana ya Mawasiliano na Miundombinu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe, Hamadi Masoud, alithibitisha kwamba anataaarifa za ujio wa meli hiyo ambayo alisema kwa kiasi kikubwa itakuwa ni ya kutoa huduma tu na siyakutengeneza faida. Meli hiyo inauwezo wa kwenda kasi ya notkomail 20.
Waziri Mwenye dhamana ya Mawasiliano na Miundombinu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe, Hamadi Masoud, alithibitisha kwamba anataaarifa za ujio wa meli hiyo ambayo alisema kwa kiasi kikubwa itakuwa ni ya kutoa huduma tu na siyakutengeneza faida. Meli hiyo inauwezo wa kwenda kasi ya notkomail 20.
Assalama Leko zako Muungwana Said S.Bakhressa na Azzam kwa ujumla!
ReplyDeleteHaya ndiyo mambo Sheikh lililobaki ni kuukamilisha ule 'Ungo' Uwanja wa Timu ya Mpira kule Chamazi-Mbagala ili na sisi wana Mbagala tuweze kujitetea dhidi ya dharau za Wanamuziki wa Kizazi kipya juu yetu kuwa Mbagala kila nyumba ni jalala!
Hiyo ni ferry
ReplyDeleteTatizo ni moja tu ambalo kwetu wakaazi wa shangani imekuwa kero kwa muda mkubwa sasa. Tatizo lenyewe ni sehemu ya kupakia na kushushia magari na abiria wa meli hiyo.
ReplyDeleteKwa sasa meli zinazosafirishia magari kwenda dar na pemba hutumia ufukwe wa hapa shangani karibu na posta na benki kuu ya biashara. Kwa vile hakuna sehemu maalum ya kuegesha magari yanayongojea kusafirishwa, sehemu hiyo huwa daima imejaa magari na kusababisha msungomano wa magari na wapita njia katika sehemu hiyo.
Ikiwa Azam nao watatumia sehemu hiyo basi naona patakuwa hapapitiki tena hata kwa miguu.
Kinachochekesha hapa ni ule mtindo wa magari kuegeshwa hapa na kusubiri hadi maji ya kupwe ili meli iweze kusogea karibu na kupakia magari, au mara nyengine meli inasubiri maji yajae kiasi ili iweze kuelea na kuondoka. Hapatumiwi watu wa taaluma ya hali ya hewa na bahari kujua ni time gani kwa siku gani kutakuwa high au low tides.
Hongera Azam, wewe kweli ni mzalendo
ReplyDeletekwani unajenga nchi, sio hao mafisadi
wanaiba na kupeleka ulaya.
Mungu akuzidishie
Amen
Ras z
ni nzuri sana afadhali.ila tunaomba kuona sehemu ya abiri au vyumbani.
ReplyDeletesi mchezo hongera sana said s bakhressa wewe ndio mbunifu wa hali ya juu
ReplyDeletehizo ndio meli zinazotakiwa kuwepo hapo nchini sio zile meli za mizigo zilizouwa raia wasiokuwa na hatia zaidi ya 2000
mungu akuzidishie zaidi ya hapo ili tuzidi kufaidika na mafanikio yako
sasa nitakuwa nikisafiri kuelekea zanzibar na suzuki yangu nikifika napiga misele mji wa amani nikimaliza narudi na suzuki yangu
big up Azam Familly.
Ahsante sana AZAM, mimi naomba ikiwezekana tuulizie kabisa kwenye Idara zinazohusika, masharti ya kwenda na gari Zanzibar na au Dar yatakuwa yepi ili kuondoa usumbufu. Mkipata tubandikie hapahap kwenye blog yetu.
ReplyDeleteSasa niuthibitisho tosha namna gani tunavyoweza kuimarisha muungano wetu wasiyopenda wanywe sumu,Ahsante ndugu baresa.
ReplyDeleteLugha iliyotumika katika kichwa cha habar hii nadhani sio sahihi.Watu hawataenda zanzibar kwa magari yao bali wataenda zanzibar pamoja na mgari yao.Kichwa cha habar mm kilinifanya nidhani kumejengwa au kutajengwa daraja lakuunganisha dar na zenji.Hivyo kichwa cha habr kinatoa ujumbe tofauti.
ReplyDeleteOngera Azam
ReplyDeletehizo notkomail no sawa km ngapi/hr. itachukua mda gani kwa safari 1?
ReplyDeletehongera sana!
notkomail 20 ni sawa na kutumia dakika ngapi toka Dar kwenda Zanzibar, habari haijakamilika kipande hiki cha speed hasa ukizingatia sie sio wataalamu wa vyombo vya majini ingekuwa kama ile ya gari ya KM/HR tungetumia general knowledge ya physics ya form two. WANAOJUA WATUJUZE
ReplyDeleteTanga na Mtwara je? Ili tukimbie Foleni na ajali za Barabarani. Pia muanzishe USAFIRI BASI MBEZI,MPAKA SLIPWAY MSASANI KUTOKA HAPO MPAKA FERRY AU NYENGINE INATOkEA KAWE AU MSASANI CINE CLUB, ILI TUKIMBIE FOLENI VITU VIDOGO TUNASHINDWA TUNAJUWA WENGINE TUKITAKA KUFANYA AZAM WANATUZUIA. PANDU
ReplyDeleteUSALAMA NAO UWEPO UOKOAJI NAO UWEPO WAWE MAKINI MSIWEKE TAMAA MBELE TU ALLAH ATUZIDISHIE NA KUTULINDA NA TUONGEZEE BIDII YA MAFANIKIO.
ReplyDeleteKigamboni sasa hivi ni kero ngoma kama hii hali ingekuwa shwari kabisa hata kwa gharama ya juu kidogo
ReplyDeleteHii nzuri, ila nakushauri uvushie watu na magari kwenda kigamboni italipa, ukipeleka znz-dar inaweza isijae na ukaishia kupata hasara, vusha kigamboni hao TEMESA wamelala usingizi biashara ipo hapo.
ReplyDeleteHongera Bakhresa huu ndio uwekezaji!
Hii ni Boat nadhani, sio Meli. Tutofautishe Ziwa na Bahari, sio kila Ziwa ni Bahari.
ReplyDeleteNawakilisha.
20 nautical miles (Nm) ni sawa na 37 km/hr
ReplyDeletehuu ndio uwekezaji watanzania wanautaka kama huyu AZAM safi sana yeye analeta hapa nyumbani lakini hawa ndugu zetu mafisadi wao wanaiba wanawapelekea hao wazungu ambao wanatuletea misaada mpaka wanatushangaa hawa jamaa vipi?bajeti yao tunawasaidia bado wanaiba,kweli akili ni nywele kila mtu anazo,nichukue nafasi ya kukupongeza AZAM,sasa issue ni namna ya kupata ajira kwenye hiyo meli
ReplyDeleteMambo ya msingi ni kujenga sehemu ya kupakia/pakua magari katika kila bandari.
ReplyDeleteTuelezwe taratibu za kwenda na magari Zanzibar itakuwaje? je Zanzibar ni kama Moro tu kuwa naenda halafu hamna masharti mengine?
Gharama zinakadiriwa kuwaje?
Je kuna haja ya kufanyba 'booking' mapema au ni kama pale Kigamboni, wa kwanza kufika ndio wa kwanza kuhudumiwa (ukiondoa mafisadi wachache wanaoruka foleni)
Shukrani sana kwa huduma hii
Muungano unahitaji watu kama hawa:
ReplyDeleteWatu muhimu katika Muungano ni wale wanaoona faida zake akiwemo Sheikh Said Seif Bakhressa!
Ndiye anatuwakilisha nchini na mwana mapinduzi mzuri, Wapinga Muungano hatuna muda wa kuwatimizia mahitaji yao!!!