Waziri wa Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo,Mh.Dkt. Fenella Mukangara (pichani) amepata ajali mbaya mchana huu maeneo ya Nzega Mkoani Tabora wakati akiwa njiani kuelekea Jijini Mwanza kwenye Ufungunguzi wa Mashindano ya Taifa ya Mchezo Vishale (Darts) yanazinduliwa leo Jijini humo.

Globu ya Jamii imefanya mawasiliano na Mh. Mukangara na kuthibitisha kupata ajali hiyo ambapo anasema chanzo chake ni kuchomekewa na basi moja la abiria (ambalo hakulitaja jina lake).

"Ni kweli tumepata ajali hapa maeneo ya Nzega Mkoani Tabora wakati tukiwa njiani kuelekea jijini Mwanza ambako leo kunafanyika ufunguzi wa Mashindano ya Taifa ya Mchezo wa Darts,tunashukuru Mungu wote tumetoka salama japo tumepata majeraka katika sehemu mbali mbali za mwili."Alisema Mh. Mukangara.

Tunaendelea kuwasiliana na Mh. Mukangara na tutaendelea kupeana taarifa zaidi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 29, 2012

    Pole mheshimiwa na wote waliohusika kwenye ajali hii.Haya sasa tuone serikali itafanyanini juu ya swala la madereva wanaoendesha magari kwa kutofuata taratibu za udereva.kwaniwananchi tumepiga sana kelele na kupoteza ndugu zetu juu ya uzembe wa madereva. WAKATI UMEFIKA WA KUBADILIKA NA SERIKALI KUFUATILIA UZEMBE WA MADEREVA.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 29, 2012

    atatibiwa na nani wakati madaktari wamegoma?.au ataenda india na nchi nyingne wanakothaminiwa wataalamu badala ya kuabudu siasa kama hapa kwetu?, au ana daktari wake anayemlipa vizuri!

    ReplyDelete
  3. Pole sana. Tatizo madereva wengi Bongo hawafuati sheria za barabarani au hawazijui kabisa! Bongo road law.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...