Nyumba ambayo imepatwa na janga la kuwaka moto usiku wa kuamkia leo ikiendelea kuteketea kwa moto huo katika maeneo ya kashai,Wilayani Bukoba Mkoani Kagera,Chanzo cha moto huo inasemekana ni mshumaa uliokua ukiwaka katika moja vyumba vililivyo ndani ya nyumba hiyo na kusababisa kuwaka kwa moto huo.hakuna mtu aliepoteza maisha katika ajali hiyo.
Kikosi cha Zima moto Mkoani Mara kikiendelea na jukumu lake la kuuzima moto huo.
Sehemu ya Mabaki ya mali za watu waliokuwa wakiinshi kwenye nyumba hiyo.
Baadhi ya wakazi wa Kata hiyo ya Kashai wakiwa katika eneo la tukuo kushuhudia.
mmoja kati ya wapangaji kwenye nyumba hio akiongea na Mdau wa Globu ya Jamii alietuletea taarifa hii wakati akisema chanzo cha moto huo na kuthibitisha kuwa ni Mshumaa uliokuwa unawaka.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 07, 2012

    Hii ni mara ya kwanza nasikia mshumaa ndio chanzo cha kuteketea nyumba. Mara nyingi utasikia ni hitilafu ya umeme, hata kama nyumba iliyoungua haikuwa na umeme. Hii 'hitilafu ya umeme' hutumika kuficha uzembe unaosababisha moto.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 07, 2012

    Huu ndiyo moyo/spirit watanzania tuliokuwa nao wa kupiga kazi tuliyoichagua kufanya. Hongora sana kikosi cha zima moto Bukoba. Viongozi wetu wangekuwa na moyo huu nchi yetu ingekuwa mahali bora pa kuishi kuliko sehemu nyingine yeyote duniani. Endelezeni moyo huu watoto wetu wafuate.

    ReplyDelete
  3. Kaka TrioJune 07, 2012

    Kazi kwlei kweli moto Kagera unazimwa na kikosi cha zima moto kutoka Mara. Ama kweli wahaya bila watani zao wakurya ni apache alolo!

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 07, 2012

    HONGERA KIKOSI CHA ZIMAMOTO, JUHUDI ZENU TUMEZIONA JAPOKUWA MMEKUTA MAJIVU HIVYO HAMKUFANYA AJIZI MKAYAZIMA.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 07, 2012

    Kuna mwaka moto uliwaka Tanga na fire ilitoka Dar

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 08, 2012

    ni kawaida, imagine wilaya ambazo hazina zima moto na makao makuu ya mkoa yako mbali na wilaya hizo, lazima sehemu yoyote zima moto ilipo karibu isaidie. cha muhimu isije ikatoka zimamoto mkoa mmoja hadi mwingine na ukakuta ina hitilafu, du!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...