Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Royal Group ya Saudi Arabia, Dkt. Sulaiman Al Fahim wakati walipokutana leo, Jumamosi, Juni 2, 2012, Ikulu Dar es Salaam. Dkt. Al Fahim ambaye ni mwenyekiti wa zamani na mmilikimwenza wa Klabu ya soka ya Portsmouth ya Uingereza yuko nchini kuangalia uwezekano wa kuwekeza katika uchumi wa Tanzania. Dkt. Al Fahim pia ndiye aliyeongoza mazungumzo na kununuliwa kwa klabu bingwa ya Ligi Kuu ya Uingereza ya Manchester City na Kampuni ya Arabuni. (Picha na fredy Maro).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 7 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 03, 2012

    Kuweni makini na watu wanaokuja na majoho toka arabuni kwa madai ya uwekezaji,ni aibu mtu anapokuja na kupata kukutana na raisi ndani ya ikulu.Huyu jamaa japo ndio alihusika katika mazungumzo ya kununua man.city na ndio gia aliyoitumia kununua portsmouth lakini hana kitu kwani timu imefilisika na inashindwa hata kulipa mishahara na imenyang'anywa pointi kumi ikasababisha kushuka daraja la tatu.kama angekua na pesa si angeokoa timu yake? Ameshindwa hata kuwalipa mishahara wachezaji Tal Ben Haim na Kanu. Waandishi wetu wa bongo jaribuni kufanya research kidogo ili mtoe habari ya pande nyingi sio kuchukua tu story na kui publish kama mlivopewa na watu wa PR

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 03, 2012

    KJ...mwambie huyo amwambie kocha wake aje aangalie vipaji vya soka Tanzania.

    David V

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 03, 2012

    anon wa kwanza:

    kwa hiyo akija na suti ni poa hata kama alifilisika.

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 03, 2012

    anon wa kwanza:

    kuwa muwazi kuwa hutaki mwarabu au isilamu, mdini mkubwa we.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 03, 2012

    sasa avae nini wewe mshamba hapo juu AVAE SUTI au awe MZUNGU? ndio wa maana??? mijitu mingine ZEROOOO

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 04, 2012

    Huyo jamaa hapo juu ni mshamba sana, na anaabudu wazungu wakati wazungu wanamuona nyani tu, pole sana kaka kwa ujinga wako mkubwa....

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 04, 2012

    Usije kusema kuwa hujui wamiliki wakiingia nchini.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...