Spika wa Bunge,Mh. Anne Makinda |
SPIKA wa Bunge Anne Makinda amewataka wabunge warudishe heshima ya Bunge kwa kuacha tabia za kupigana vijembe wakati wanapochangia Bajeti ya Serikali.
Makinda amesema michango ya wabunge ni muhimu katika kuboresha Bajeti ya Serikali, hivyo kama wakiacha kuchangia na kuingia kwenye malumbano ya kisiasa, hawawezi kuisaidia Serikali na wananchi waliowatuma.
Makinda alitoa mwito huo jana baada ya kipindi cha maswali na majibu baada ya siku mbili za mjadala wa bajeti hiyo kutawaliwa na malumbano ya kisiasa hali iliyowalazimisha wabunge kutoa lugha za kuudhi.
Spika huyo alisema amepokea simu nyingi zinazowashutumu wabunge kuhusu hali iliyojitokeza katika mjadala wa bajeti kuanzia Jumatatu.
“Nimepokea simu wananchi wanasema wabunge hamjadili bajeti ila mnachofanya hapa mnalumbana,” alisema Makinda.
Alisema wabunge wakiendelea kuonesha ubingwa wao wa kupiga siasa katika kujadili bajeti hiyo, wananchi waliowatuma watasikitishwa na hali hiyo.
Alisema ushauri wa wabunge ni muhimu ili Serikali ijue iboreshe wapi na ipunguze wapi matumizi ili wananchi wapatiwe bajeti nzuri.
“Wananchi wanawaona mmoja mmoja mnayofanya hapa, nawaombeni mrudishe heshima ya Bunge,” alisema Makinda.
Kiongozi huyo pia aliwaka wabunge hao wajihurumie wenyewe kwa mambo ya ajabu wanayofanya ukumbini ya kuonesha ubingwa wa kupiga siasa.
Akiahirisha Bunge baada kumalizika kwa kipindi cha asubuhi, Spika Makinda alieleza kuridhishwa na michango ya wabunge waliochangia kuanzia asubuhi.
Waliochangia asubuhi, walikuwa wabunge 15 ambao ni Yussuf Nassir (Korogwe Mjini –CCM); Salvatory Machemli (Ukerewe – Chadema); Henry Shekifu (Lushoto – CCM); Luhaga Mpina (Kisesa – CCM); Dk Kebwe Stephen (Serengeti – CCM); Albert Ntabaliba (Manyovu – CCM); Desderius Mipata (Nkasi Kusini – CCM) na Danstan Kitandula (Mkinga – CCM).
Wengine ni Meshack Opulukwa (Meatu –Chadema); Kidawa Himid Saleh (Viti Maalumu – CCM); Dk Titus Kamani (Busega – CCM); Mariam Kisangi (Viti Maalumu – CCM); Augustino Masele (Mbogwe – CCM) na Masoud Abdalla Salum (Mtambile – CUF).
Wakati huo huo, Makinda alisema Muswada wa Sheria ya Fedha ambao awali ulipangwa kupitishwa kesho baada ya kupitishwa kwa Bajeti ya Serikali, sasa utasubiri hadi mwishoni mwa Mkutano wa Nane wa Bunge.
Spika alisema wamefanya hivyo baada ya utafiti kubaini kuwa mabunge mengi ya Jumuiya ya Madola yana utaratibu wa kupitisha Muswada wa Sheria ya Fedha na Muswada wa Sheria ya Matumizi mwishoni kabisa mwa mjadala wa bajeti.
Alisema kwa kuzingatia ombi la Serikali na wabunge walio wengi pamoja na maoni ya Kamati ya Bunge ya Fedha na Uchumi, muswada huo sasa utapitishwa mwishoni mwa mkutano unaoendelea kwani bado Serikali inaweza kukusanya mapato kabla ya muswada huo kupitishwa.
Kutokana na mabadiliko hayo, Makinda alisema sasa mjadala wa bajeti utakuwa wa siku tano badala ya nne na hivyo utahitimishwa kesho Ijumaa.
Madame Speaker if you were in England or any other developed country someone can request to know who actually rang you and at what time under Freedom of Information. Usidanganye watu, who in Bongo would dare ring your office to complain, it would be a waste of his/her time.
ReplyDeleteI think MPs are alllowed to say anything they want in Parliament, they have the freedom of Parliament to do so. Visit England, Australian parliaments and see what the leaders are called in Parliament, you will have a shock of your life.
People are paid to actually research on their lives and all is brought into Parliament if they have ever done sinister things. The biggeer the number oppostion MPs, you will have learn how to live with it, I can't wait for 2015.
Mheshimiwa Makinda, do not compare your parliament with other Parliaments in the West. They do not have time to waste for 3 months going through each Depts budget. I witnessed one recently, it took the Minister only 30 minutes to present. It is consolidated and contained all the information on every dept or ministry. A parliamentary session never goes for more than 2 weeks, yours for 3 months, what a u debating if you have passed the Treasury budget which has all the ministries estimates?
ReplyDeleteVijembe vinaanza baada ya spika kuruhusu kwa namna inayoashiria upendeleo, upande wa chama tawala kusema watakacho kuhusu upinzani huku akiwazuia wapinzani kutofanya hivyo. Matokeo yake wapinzani wanajibu kwa hasira zaidi ndipo vijembe vinaanza. Spika ndiye anatakiwa kubadilika kwanza.
ReplyDelete