Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF) unawatangazia wadau wake kuwa, Mkutano Mkuu wa wadau utafanyika tarehe 29 Juni 2012 kuanzia saa mbili asubuhi hadi saa kumi na moja jioni katika hoteli ya Blue Pearl - Ubungo Plaza, Dar es salaam.
Madhumuni ya Mkutano huu ni kutoa taarifa ya mwaka ya Mfuko na kutathmini maendeleo na changamoto zinazokabili Mfuko na sekta ya Hifadhi ya Jamii kwa ujumla.
Tafadhali thibitisha ushiriki wako kwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu makao makuu, Dar es Salaam.
“PSPF - TULIZO LA WASTAAFU”
Kaimu Mkurugenzi Mkuu
Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma,
Makao Makuu,Golden Jubilee Towers, S.L.P 4843. Dar-es-Salaam.
Simu: +255222120912/52 au +255222127375 /6
Nukushi: +255222120930
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...