![]() |
JIMMY DAVID NGONYA 22 June 1942-23 July 2011 |
Ni mwaka mmoja sasa tangu mpendwa wetu ulipotutoka ghafla asubhi ya tarehe 23/07/2011. Unakumbukwa sana na mke wako, watoto, wajukuu, ndugu na marafiki upendo, ucheshi na ukarimu wako bado vinaishi ndani yetu.
Ibada ya kumbuku itafanyika tarehe 29/07/2012 katika kanisa la Moravian karikooo, Imani Mission Congregation Reading. St Andrews URC Church, London Road, Reading, Berkshire RG1 5BD 02.00 pm na Kijijini Mibula, Tukuyu tarehe 11/08/2012.
BWANA AMETOA, BWANA AMETWAA, JINA LA BWANA LIBARIKIWE
Msijisumbue kwa neno lolote;bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu. Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.Mkishukuliana, na kusameheana, mtu akiwa na sababu ya kumlaumu mwenzake kama Bwana alivyowasamehe ninyi vivyo na ninyi.Maneno yenu yawe na neema siku zote yakikolea munyu, mpate kujua jinsi iwapasavyo kumjibu kila mtu. Na amani ya Kristo iamue mioyoni mwenu;ndiyo mliyoitiwa katika mwili mmoja; tena iweni watu wa shukrani.Mkipendana mtazishika amri zangu.Nami nitamwomba Baba,naye atawapa msaidizi mwingine,ili akae nanyi hata milele;ndiye Roho wa kweli;ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea,kwa kuwa haumwoni wala haumtambui;bali ninyi mnamtambua;maana anakaa kwenu,naye atakuwa ndani yenu.Sitawaacha ninyi yatima;naja kwenu.
PUMZIKA KWA AMANI
MPENZI, BABA, BABU NA RAFIKI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...