MKOA wa Mara umekamilisha tayari umechukua hatua za haraka za kuhakikisha zoezi la Sensa ya watu na makazi linafanikiwa kama lilivyopangwa katika visiwa 30 ambavyo vimo ndani ya ziwa Victoria.
 
Mratibu wa Sensa mkoa wa Mara Bw Ramadhan Mbega (pichani) ,amesema kuwa mbali na kuyabainisha maeneo hayo pia imetenga maeneo ya kuhesabia watu katika maeneo ya hifadhi za taifa ya Serengeti na mapoli ya akiba yanayopakana na hifadhi hiyo.
 
Alisema kwa mkoa Mara,maeneo 3335 yametengwa kwaajili ya zoezi hilo la Sensa ya watu na makazi ambalo linatarajia kufanyika nchini kote kuanzia Agosti 26 mwaka huu huku kila halmashauri ikifanya maandalizi ya kufundishia mawakala watakaofanya kazi hiyo.
 
Hata hivyo Bw Mbega,amewataka wananchi wa mkoa wa Mara kuachana na dhana potofu ya baadhi ya watu kuwa endapo watahesabiwa katika zoezi hilo wanaweza kupoteza maisha ama kushindwa kuzaa.
 
Bw.Mbega aliongeza kuwa si kweli kuwa watu wakihesabiwa watashindwa kuzaa au kupoteza maisha na kuongeza kuwa zoezi hilo linalenga kuwezesha taifa kupata takwimu sahihi za watu na makazi kwaajili ya kuwahudumia vema wananchi wake.
 
Mbali na hivyo mratibu huyo alimpongeza mkuu wa mkoa wa Mara Bw.John Tuppa kwa kuwa mstari mbele kuhamasisha wananchi kuhusu zoezi hilo la Sensa

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...