TASWIRA MBALI MBALI ZA MATOKEO YA MGOMO WA MABASI YA USAFIRISHAJI KATI YA ARUSHA NA MOSHI KAMA WANAVYOONEKANA ABIRIA WAKIWA KWENYE STAND KUU YA MABASI JIJINI ARUSHA WAKITAFUTA USAFIRI KAMA WALIVYOKUTWA NA KAMERA YETU.

 MGOMO HUO BADO UNAENDELEA KWA SIKU YA TATU SASA HALI INAYOLETA USUMBUFU KWA ABIRIA HAO AMBAO HATA INAWABIDI KUINGILIA MADIRISHANI KWENYE MABASI MACHACHE YANAYOFANYA KAZI, NA WENGINE KUIBIWA. INASEMEKANA MGOMO HUO UMETOKANA NA HALMASHAURI YA MANISPAA YA MOSHI KUPANDISHA USHURU KUTOKA 1000 -2000 BILA YA KUFIKIA MUAFAKA NA WAMILIKI HAO WA VYOMBO VYA USAFISHAJI MJINI HUMO.
Picha na Mahmoud Ahmad, Arusha





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 10, 2012

    Mateso yote haya yanatokana na kukosekana kwa watawala ambao aidha hawana dhamira ya kuifanyia kazi dhana ya utawala bora au hawana uelewa wa dhana yenyewe. Utawala bora unakita katika misingi ya ushirikishaji (participatory and involvement) wadau mbali mbali katika maamuzi yanayowagusa. Inashangaza kuona ubabe ikitawala hadi sasa na matokeo yake ni usumbufu usiokuwa na sababu kwa wananchi.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 11, 2012

    Kwani huo mgomo umetokea kwenye basi la Mtei pekee?

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 11, 2012

    Ni kweli Juu ya hoja hapo juu. Usumbufu mkubwa umetokea kwa mgomo huu kudumu kwa sikuhizo bila ufumbuzi wa haraka_Wanaokwenda kazini, mashuleni, hospitali, kazini, mashambani na kwengineko imekuwa adha kubwa! Wao wana magari yao wakipeta juu kwa juu bila shida ! Aidha uchumi umeyumba - mauzo mengi yamedoda kwani wadau wanshindwa kufikia masoko na huduma- mfano wauza mafuta wamekiona - kutoa gari takribani 200 si mchezo! Je nani atatulipa adha hii tuloipata! Mheshmiwa mstahiki Meya na Mkurugenzi manispaa mtujibu.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...