Kufuatana na kifungu nambari 41 cha Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta ya mwaka 2010, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania inapenda kufahamisha umma kwamba orodha ya Misimbo ya Posta au ‘postikodi’ za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imechapishwa kupitia Gazeti ya Serikali Notisi nambari 220 ya tarehe 22 Juni 2012.
Msimbo wa posta (Postikodi) ni mkusanyiko wa tarakimu inayotambulisha eneo la usambazaji wa barua na kwa Tanzania eneo linalotambulishwa ni Kata kwa Tanzania Bara na Wadi kwa Zanzibar.
Kazi hii ya kitaalamu ya kugawa misimbo ya posta imefanyika baada ya utafiti wa muda mrefu ambao umehusisha watalaamu mbalimbali. Ili kuufahamu mfumo wa Msimbo wa Posta wa Tanzania, vigezo vifuatavyo vimetumika kama ilivyofafanuliwa hapa chini.
mpango mzuri sana huu
ReplyDeleteasante kwa taarifa