Wachezaji wa Simba (Wabunge) wakishangilia ushindi baada ya kuwafunga watani wao wa Yanga (Wabunge) kwa penalti 3-2.
Yanga baada ya kipigo hicho.

Hivi ndivyo hali ilivyokuwa katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam katika mtanange wa watani wa jadi Simba na Yanga (Wabunge) wakati wa TAMASHA LA MATUMAINI ambapo wabunge wapenzi wa timu ya Simba wameibuka kidedea kwa penalti 3-2. Simba wamefunga penalti 3 wakati Yanga wakifunga 2.

(PICHA ZOTE NA GPL)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 08, 2012

    Wana yanga mmeona kiwingu kimeanza kutanda?jina linazidi kuchafuka sasa subirini mkutane na mnyama wa ukweli namaanisha wekundu kamili kwenye ligi au mashindano ya kagame cup naona safari hii huyo kocha anyoe upara na ajiandae kwenda kifanya biashara mitaa ya kariakoo Na kipigo kijacho hata cha mbwa mwizi kinanafuu mtatimua hadi wanachama

    ReplyDelete
  2. Inafurahisha na kupendeza kwa waheshimiwa wabunge kujichanganya, hii ndio Tanzania tunayoitaka yenye amani na utulivu, kuna nchi nyingine muda wa kucheza ndombolo haupo,mtu anawaza wapi akimbiziye uhai wake hata familia yake haijui ilipo. Huu ni mwanzo mwema, matumaini yanapatikana,waheshimiwa mkirudi kule nyuma enzi za baba yetu wa Taifa, waheshimiwa wote walikuwa saizi moja,walipendwa na kila mtu. Utamaduni wa kujibagua kwa vyeo ni sumu usipewe nafasi, michezo haijui cheo wala fukara wote tushirikiane kuliongoza taifa. Yanga juu, mbele daima, simba ivunjwe ichanganywe na yanga tupate Timu kubwa na nzuri itatufikisha mbali.
    mdau,

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...