Baadhi ya Wanzania 38 waliokuwa wakimbizi Jijini Mogadishu wakielekea sehemu ya mapokezi mara baada ya kushuka katika ndege la Umoja wa Mataifa iliyowaleta nyumbani wakiwa na wake zao waliooa nchini Somalia baada ya kuishi huko kwa miaka 11,walikimbia vurugu za Januari 26/27 mwaka 2001.
Baadhi ya Watanzania waliokimbilia jijini Mogadishu nchini Somalia mwaka 2001 wakiwa katika Ofisi ya Uhamiaji Zanzibar. Wa kwanza ni Mohammed Adam (38) akiwa amembeba mwanae mara baada ya kuwasili uwanja wa ndege wa kimataifa wa Abeid Amani Karume,wanaotazama kamera ni baadhi ya wake wa Watanzania hao ambao ni raia wa Somalia waliowasili wakitokea Mogadishu Somalia na ndege ya Umoja wa Mataifa inayoshughulikia huduma za kibinadamu.
Watanzania waliokuwa wakimbizi katika kambi ya Mogadishu wakielekea kupanda mabasi maalum yaliyoandaliwa na Shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa baada ya kuwasili Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume,Zanzibar.(Picha na Juma Mohammed,MAELEZO Zanzibar).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 07, 2012

    pamba walizopiga baab kubwa. halafu kila mmoja kaja na mwanamke wa kisomali.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 07, 2012

    KARIBUNI NYUMBANI

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 07, 2012

    Kumbe Somali mambo mazuri bwana!!

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 08, 2012

    somalia kama sio vita basi tanzania ingekuwa ipo chini ya somalia kwa umasikini, tanzania ni number 4 duniani kwa umasikini but kama hizo nchi tatu zitakuwa hazina migogoro ya kupigana na vita basi tanzania itakuwa number 1 duniani kwa umasikini

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 09, 2012

    Hawa watu ndio wanaotupakazia sana katika Jumuia za Kimataifa.

    Tokea lini Tanzania tukawa na Wakimbizi?

    Angalia sasa wametahayari, wanarudi nchini wamezusha mambo kuwa kuna hali hatarishi nchini wakakimbia, UN imefanyia kazi taarifa ikaona hakuna ukweli wa madai yao sasa imewaingiza kwenye ndege imewarudisha!

    Serilaki ipo tulivu inawakaribisha kwa mikono miwili!

    Tena hawa jamaa ikiwezekana wapewe mikopo ya Saccos ili wapate kazi za kufanya waache uchochezi wa kutuchafua Tanzania Kimataifa!

    ReplyDelete
  6. AnonymousJuly 09, 2012

    Ukimbizi gani nyie Watanzania, semeni mmekimbia kwa njaa iliyotokana na uvivu wenu binafsi tu!

    Mbona wenzenu waliopo Tanzania Bara wanafanya shughuli zao na hawana ubwege kama wenu mliofanya?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...