MAKAMU WA RAIS WA NCHINI AFRIKA KUSINI,KGALEMA MOTLANTHE ( KATIKATI) AKIANGALIA MOJA YA KABURI LA MPIGANIA UHURU WA ANC , ENEO LA MAZIMBU,MJINI MOROGORO.

Na John Nditi .

Makamu wa Rais wa Afrika ya Kusini, Kgalema Motlanthe, Julai 9, mwaka huu alifanya ziara ya siku moja Mjini Morogoro, ililiyokuwa mahusisi kwa ajili ya kutembelea eneo la Mazimbu, ilikuwa kambi ya wapingania uhuru wa Chama cha ANC.

Ziara hiyo ilikuwa ni sehemu ya kuadhimisha miaka 20 tangu harakati za ukombozi wa Afrika Kusini zilipomalizika ,katika Kambi hiyo , ANC iliacha majengo na vitu mbalimbali vilivyokabishiwa Serikali ya Tanzania, pia yapo makaburi kadhaa walimozikwa mashujaa hao, ambapo Makamu huyo wa Rais aliweza kuzuru na kuweka shada la maua katika mnara wa kumbukumbu ya wapigania uhuru hao pamoja na kupanda mti.

Kabla ya kufanya shughuli hiyo,alipata fursa ya kutembezwa maneo mbalimbali yakiwemo majengo yaliyokuwa yakitumiwa na wapigania uhuru hao, ikiwemo Shule ya Msingi na Awali, Shamba la Mifuko, Kiwanda cha samani pamoja na Hospitali .

MAKAMU WA RAIS WA AFRIKA YA KUSINI AKITOA HESHIMA BAADA YA KUWEKA SHADA LA MAUA KWENYE MOJA YA KABURI LA MPIGANIA UHURU WA ANC , ENEO LA MAZIMBU,MJINI MOROGORO.
MAKAMU WA RAIS WA AFRIKA KUSINI , KGALEMA MOTLANTHE, AKIPANDA MTI ENEO LA MAKABURI YA WAPIGANIA UHURU WA ANC , MAZIMBU, MJINI MOROGORO.
MAKAMU WA RAIS WA AFRIKA KUSINI AKITOKA KUTEMBELEA HOSPITALI YA MAZIMBU AMBAYO ILIKUWA IKITUMIWA NA WAPIGANIA UHURU WA ANC, AMBAPO KWA SASA IMEKARABATIWA NA KUONGEZWA MAJENGO MAPYA.
BAADHI YA RAIA WA AFRIKA KUSINI WALIOAMBATANA NA MAKAMU WA RAIS WA NCHI HIYO HAPA NCHINI.
BURUDANI KWA MGENI RASMI,MAKAMU WA RAIS WA AFRIKA KUSINI ALIPOTEMBELEA SHULE YA MSINGI CHIEF ALBERT LUTHULI, MAZIMBU MJINI MOROGORO.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Mmmmh!

    Kaka. Huyo Raia wa Afrika ya kusini mwenye sketi nyekundu na mistari myeusi kwa chini na miwani myeusi ya jua vipi hukubahatika kupata kontakti zake kaka?

    Daah!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...