MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, leo inatarajia kutoa hukumu ya Kesi ya Uhujumu Uchumi na Kuisababishia Serikali hasara ya Euro 2 milioni, inayomkabili aliyekuwa Balozi wa Tanzania, nchini Italia Profesa Costa Mahalu na Ofisa Utawala wa ubalozi huo, Grace Martin.

Profesa Mahalu na Martin wanakabiliwa na mashtaka sita yakiwamo ya uhujumu uchumi na kuisababishia Serikali hasara ya Euro 2,065,827.60, katika mchakato wa ununuzi wa jengo la Ubalozi wa Tanzania nchini Italia.

Hukumu ya kesi hiyo iliyokuwa ikinguruma mahakamani hapo kwa miaka kadhaa sasa, inatarajiwa kusomwa leo na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Ilvin Mugeta ambaye amekuwa akiisikiliza.

Awali, hukumu hiyo ilipangwa kusomwa Julai 11, mwaka huu lakini iliahirishwa kutokana na Hakimu Mugeta kukabiliwa na majukumu mengine. Kesi hiyo iliahirishwa na Hakimu Mkazi, Aloyce Katemana na kupanga kuwa hukumu hiyo itasomwa leo.

Kiongozi wa jopo la mawakili wa washtakiwa hao, Mabere Marando alisema jana kwamba anaamini kesi hiyo ambayo imechukua muda mrefu, leo inafikia mwisho kwa Mahakama kutoa hukumu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...