Kinkwin Creative Solutions, mabingwa wa kuweka copy block kwenye DVD wamekuja na ofa ya BUREEE kabisa ya kumwekea msanii mmoja kazi yake copy block ya nguvu na hivyo kumsaidia kazi hiyo isihujumiwe na vishoka kirahisi. Ofa hii ni kwa kazi yote nzima ya msanii yaani  DVD zote za kazi moja zitawekewa copy block buree hata kama kazi yenyewe itahitaji copy zaidi ya milioni moja

Kama unabisha  basi JARIBU UWEZO WETU. Wasiliana nasi ujionee kazi ambazo tumeziwekea copy block na wateja wetu wameridhika nazo. usikubali kuandikia mate na wino upo. Kuona ni kuamini. Njoo ujionee

Kampuni yetu imekuwa ikitoa ofa nyingi za bure ikiwa ni pamoja na website (unlimited bandwidth) za bure, ku shoot filamu ama video bure , kuweka copy block bure, kumtengenezea mteja post effects bure, na mambo mengi.

Unaweza kuwasiliana nasi kwa njia mbalimbali, ikiwa ni pamoja na cellphones; 0714892694/ 07654400270 / 0713830772 
- Facebook; kinkwin csolutions 
Waweza pia kutembelea website yetu; Kinkwin.com 

USIKUBALI OFA HII YA BURE IKUPITE BURE!

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. Waseme Mfano wa kazi walizoblock, tutafute locally, tujaribu ku-ublock then ndio tunaweza kusema kama kweli wanauwezo wa kublock.

    ReplyDelete
  2. If a DVD can be played using a DVD player or a computer, then it can be copied.Its just a question of, can it be done easily or its difficult.Any safe can be cracked, its just depends on your skill.Hawa jamaa wanablock hizi kumzuia Hamisi Juma asikopi.

    ReplyDelete
  3. Hiyo Block yenu mmetoa ahera? nothing is imposible...!

    ReplyDelete
  4. Nakubaliana na anaye sema kwamba hakuana kisichowezekana kuvunjwa. Hata mwizi wa duka anaweza kuvunja mlango wenye kofuli. Lakini hakuna mtu anaye acha duka bila kulifunga kwa kofuli kisa eti hata ukiweka kofuli mwizi ata vunja. Wengine wanaweka hata mlinzi na kumlipa lakini bado wizi unaendelea kuwepo. Swali letu ni kuwa, Je basi watu waendelee kutokuweka copy block kwa sababu bado vishoka wanaweza kuivunja?

    ReplyDelete
  5. Watanzania hata uwaambie nini watabisha tu. Sijui mitazamo yetu ipoje. Hawa jamaa sio wa kwanza kuweka copy block. Ni jambo la kawaida dvd kutoka nje zinakuwa na copy block. Sasa kuulizia sijui zinatoka ahera ama wapi je ni kwa vile ni Mbongo amesema? Wenyewe wamesema ukipenda ukajaribu kazi zao. Cha msingi ni kuulizia kama ni kweli ama ni uongo.

    NI ukweli kuwa hakuna kisicho kopika ukizingatia wezi wenye utaalam wanaweza kuiba chochote hata kama kuna ulinzi wa namna gani. Lakini jamaa wenyewe wamesema kishoka hawezi ku copy kwa urahisi,wakiwa na maana kwamba Kishoka atahangaika lulikoni ile anachukua dvd na kuipachika kwenye deki ama computer na kuanza kurudufu.
    Mimi kweli ninawapa Kinkwin Shavu na kama kweli wanafanya kazi hii vizuri basi hongera zao

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...