Kundi la Simba likiwa limepumzika chini ya mti katika mbuga ya Hifadhi ya Taifa ya Wanyama ya Serengeti ambayo hivi sasa ina wageni wengi kwa kuwa ni msimu wa kutembelea mbugani, japo nyumbu wengi wako nchi jirani kwa mapumziko yao ya miezi miwili kila mwaka kabla ya kurejea tena nyumbani mnamo mwezi wa Oktoba katika kile kiitwacho  the Great Animal migration
Juu mtini kuna simba mwingine kajiopumzisha kwenye tawi
Aghalabu simba wapanda miti huonekana sehemu za Hifadhi ya Manyara na hawa wa Serengeti wameonesha kuwa nao wanaweza kupanda miti bila matatizo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. SHUKRANI NYINGI KWA ALIYELETA PICHA HIZI, JAMANI MIE NAPENDA SANA WANYAMA HASA KATIKA TASWIRA HII AMBAYO NI TAABU KUIONA UKIENDA MBUGANI, SI WOTE WENYE KWENDA HUKO WANABAHATIKA KUWAONA WANYAMA WOTE NA KATIKA MIKAO HIYO, AHSANTE TENA, ENDELEENI KUTULETEA VITU KAMA HIVI VYA NCHINI PETU ILI HATA KAMA HATUENDI WALIKO LAKINI TUNAJUA WAKOJE KATIKA PICHA.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...