Waziri wa Katiba na Masuala ya Sheria, Mhe. Mathias Chikawe ( Mb ) akipitia kwa mara ya mwisho hotuba yake kabla ya kuisoma, wakati wa mkutano wa kilele wa Umoja wa Mataifa uliokuwa ukajadili Utawala wa Sheria katika Ngazi ya Kimataifa na Kitaifa, katika hotuba yake katika mkutano huo ambao ulifunguliwa na Katibu Mkuu, Ban Ki Moon, na kuhutubiwa na Viongozi wakuu wa nchi na serikali wakiwamo Mawaziri kutoka nchi 80, alielezea namna ambavyo Jamhuri ya Muungano imekuwa ikizingatia utawala wa sherika katika ngazi ya taifa, kanda na kimataifa na akaelezea pia mchakato unaoendelea wa maandalizi ya Katiba mpya. wengine katika picha kuanzisha kulia ni Mhe. Abubakari khamisi Bakari,(Mb) Waziri wa Sheria na Masuala ya Katiba kutoka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe, Musa Hassan Mussa ( Mb) kutoka Zanzibar na waliokaa nyuma ni wataalam wa sheria.
Mhe. Mathias Chikawe ( Mb) akihutubia Mkutano wa Kilele wa Umoja wa Mataifa uliokuwa ukijadili ajenda ya Utawala wa Sheria katika ngazi ya Kitaifa na Kimataifa. Mkutano huo wa Siku Moja ulifanyika siku ya Jumatatu hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa. 


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...