Mwenyekiti wa Salasala Vision Group (SVG) chja Salasala, Dar es salaam, Yahaya Mbanka akiongea katika hafla ya kukabidhi gari la polisi la doria ambalo kikundi hicho kilichanga zaidi ya shilingi milioni 2 kwa ajili ya matengenezo
  
Mkuu wa Polisi Wilaya ya Kawe, Gilles Muroto akizungumza katika hafla hiyo.
 Waendesha bodaboda wa kituo cha Mbuyuni Kunduchi nje kidogo ya jijini Dar es Salaam wakiwa katika hafla ya kukabidhiwa vizibao 100 vilivyotolewa na SVG kwa ajili ya kuwatambua wakati wakiwa katika maeneo yao ya kazi hususani katika eneo la Salasala
 Baadhi ya Askari wa doria waliohudhuriua hafla ya makabidhiano ya gari la Polisi
  
Inspekta a Modesta Msome akitoa maelekezo kwa waendesha bodaboda wa kituo cha Mbuyuni ili kujua umuhimu wa kufuata sheria za usalama barabarani wakati wa hafla ya kutoa vizibao 100 kwa waendesha pikipiki wa eneo la Salasala, mwishoni mwa wiki
 Mkuu wa Polisi Wilaya ya Kawe, Gilles Muroto akimvisha mwendesha bodaboda, Patson Agustino moja kati ya vizibao maalum 100 vilivyotolewa na kikundi cha Salasala Vision Group kwa ajili ya kuwatambua waendesha pikipiki wa eneo hilo.
 Gari la Polisi lililofanyiwa matengenezo na SVG

Mkuu wa Polisi Wilaya ya Kawe, Gilles Muroto akipokea gari la doria la Polisi lenye namba za usajili T332 ANV kutoka kwa Mwenyekiti wa Salasala Vision Group (SVG), Yahaya Mbanka baada ya kikundi hicho kujitolea zaidi ya sh. milioni 2 kwa ajili ya kulifanyia matengenezo gari hilo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. SVG ni mfano wa kuigwa, keep it up guys. hiyo ni changamoto kwa umma kuwa si kula kitu tutegemee serikali. wanachi pia tunatoe michango yetu kwa maendeleo ya jamii. Mbona makanisani na misikiti tunatoa michango mingi ambayo hata mingine hatujui matumizi yake? Wa TZ wenzangu tuisaidie serikali yetu kwa manufaa yetu na vizazi vijavyo.

    ReplyDelete
  2. rushwa za wazi hizo.
    tunazibariki kwa kuzipigia makofi.

    ReplyDelete
  3. Eneo la salasala lilijulikana kama kandahal kwa sababu za uhalifu wa kupiliza sasa tunapumua kidogo..kumbuka tukio km la kuuwawa kwa Prof.Mwaikusa,Mtui na Gwamaka na mengine mengi yamerudisha nyuma maedeleo ya familia na taifa kwa ujumla.Leo hii tumejichangisha na kulitengeneza gari ambalo lilikua bovu ili kusaidia patrol za maeneo yetu bado kuna pumbavy anasema tumetoa rushwa.Wewe unaesema hivyo si ajabu mtaaa unaokaa vibaka ni wengi na hujachukua hatua yoyote ya kukabili tatizo.Heshimu michango a wengine kwa ajili ya jamii nzima tafadhali.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...