TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UTATUZI WA MGOGORO WA UONGOZI KATIKA CHAMA CHA SKAUTI TANZANIA
1.0 Chama Cha Skauti ni asasi isiyo ya kiserikali ambayo hutambulika kote duniani na mwanzilishi wake duniani ni Marehemu Lord Robert Baden Powell ambaye aliweza kuwaunganisha vijana wa rika mbali mbali duniani. Kwa Tanzania chama cha Skauti kilianza kutambulika katika medani ya kimataifa tokea mwaka 1963. Aidha chama cha Skauti Tanzania kwa sasa kinaendeshwa kwa mujibu wa katiba yake ya mwaka 1997.
Lengo kuu la Skauti ni kuwatayarisha vijana na kuwajenga katika maadili mema ili waweze kuwa waaminifu, wazalendo, rafiki wa wote, watiifu, wachangamfu, nwaangalifu na kuwa raia safi katika mawazo, maneno na vitendo.
Wanachama wa chama hiki wengi wao ni watoto na vijana kuanzia umri wa miaka 5-11 (Cubs), miaka 11-15 (Juniors), miaka 16-18 (Seniors) na miaka18-26 (Rovers). Wanachama walio katika umri huo wanakuwa bado wapo shuleni na vyuoni. Watu wazima (Adults) pia wanaweza kuwa wanachama wa Skauti kwa mujibu wa katiba.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...