1. KUTOKANA NA MHESHIMIWA WAZIRI NA NAIBU WAKE KUWA NJE YA OFISI, KATIBU MKUU WA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI AMEPOKEA RISALA YA WAISLAMU NA KWAMBA ATAIFIKISHA KWA WAZIRI MARA TU ATAKAPORUDI NCHINI.
2. KATIKA MAZUNGUMZO KUNA MANENO KUWA KUNA WAISLAMU WAMEWEKWA NDANI KUTOKANA NA ZOEZI LINALOENDELEA LA SENSA. KATIBU MKUU WA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI, AMETOA AMRI KWA RPC WOTE KUSITISHA UKAMATAJI WA WATU KUTOKANA NA ZOEZI LA SENSA NA KWAMBA WATUHUMIWA WALIOKAMATWA WAACHIWE KWA DHAMANA.
3. MAMBO MENGINE YOTE YALIYOTAJWA KWENYE RISALA YA WAISLAMU YATASHUGHULIKIWA MARA BAADA YA WAHESHIMIWA MAWAZIRI WENYE DHAMANA HIYO KURUDI NA MTAJULISHWA.
TAMKO LIMETOLEWA NA,
Signed
MBARAK M. ABDULWAKIL
KATIBU MKUU
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI.
07 Septemba, 2012
Usuli: Leo tarehe 07 majira ya alasiri, baadhi ya waumini wa madhehebu ya Kiislamu waliandamana hadi Makao Makuu ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi wakiwa na hoja mbalimbali ambazo waliziandika kama Risala kwa lengo la kuziwasilisha kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi. Hata hivyo Waziri na Naibu wake wako safarini hivyo Risala hiyo ilipokelewa na Katibu Mkuu wa Wizara, Mbarak Abdulwakil, ambaye baada ya majadiliano alitoa tamko hili hapa juu kwa niaba ya Waziri.
(Imesambazwa na Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi)
Kukamata watu hakutasaidia chochote, set them free.
ReplyDeleteTunakoelekea si kuzuri ee Mola inusuru tanzania. All i know sisi ni masikini sana tusiige kinachofanyika nchi nyingine. We will never know kidogo tulichonacho ni muhimu sana mpaka tupoteze tukipoteze na tukikipoteza majuto yake ni makubwa na kukipata tena ni almost impossible kuna nchi nyingi sana wish to have what we have sisi tunachezea tulichonacho. haya maandamano mema na kudai kwema hizo haki.
Waziri akisafiri si Naibu anakaimu???
ReplyDeleteHii imekaaje
safi sana mdau hapo juu umesema kitu cha maana kabisa
ReplyDeletewaachieni hao raia wa kitanzania wana haki ya kuchagua walitakalo kwenye nchi yao
serikali acheni kutesa raia wenu pasipo na sababu maonevu mpaka lini?
na huyo mheshimiwa waziri inakuaje anasafiri na naibu wake? ina maana ofisi imefungwa mpaka watakaporudi kutoka safari?
chonde chonde viongozi wetu mnapotupeleka pabaya sana tanzania inawaka ndani pindi siku huo moto utakapotoka nje nafikiri hatopatikana wa kuuzima
mungu ibariki tanzania.
Kama wamevunja sheria kwanini wasikamatwe?? Wizara ilitoa onyo kuwa ni kosa la jinai ikimkuta mtu hataki kuhesabiwa. Sasa inakuwaje waliokamatwa waachiwe? Je wengine waliokamatwa ambao sio waislamu nao itakuwaje?
ReplyDelete