Na Mwandishi Maalum, New York
Mkurugenzi wa  Kitengo cha Polisi katika Idara ya Operesheni za Ulinzi wa Amani  ya Umoja wa  Mataifa ( DPKO)  Kamishna  Ann-Marie Orler, ameiopongeza Tanzania kwa kuwa miongoni mwa nchi ambazo zimeitikia vema wito wa kuchangia  kwa idadi kubwa askari polisi wanawake. Askari  Polisi wanawake wanahitaji sana katika Operesheni za Ulinzi wa Amani    kutoka na umuhimu wao katika kushughulikia masuala muhimu yanayohusu wanawake na watoto wa kike . 

Umuhimu wao umemlazimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa  kujiwekea lengo  la kuhakikisha kwamba ifikapo mwaka 2014 idadi ya askari wanawake katika operesheni za kulinda amani  inafikia asilimia 20 ya askari polisi wote.  Kwa sababu hiyo    Kitengo cha Polisi cha   Umoja wa  Mataifa, kimezitaka nchi zote ambazo zinaombwa kuchangia askari polisi  zihakikishe kwamba kuna kuwa na uwiano sawa kati ya wanaume na wanawake na kwamba watatoa kipaumbele kwa wanawake katika uteuzi wao kwa kuzingatia pia uwezo  na sifa zilizoainishwa na  Umoja wa Mataifa na si kwa sababu tu  ni mwanamke  polisi. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Askari wa pili kushoto mstari wa kwanza amechapia

    ReplyDelete
  2. Maafande wa Kike si mchezo !

    Usije ukaomba kukamatwa na Askari wa kike, lohhh mbona utakoma?

    Ilikuwa Jumamosi ilikuja basi Doble coaster ya kuzuka haina ruti pale Stesheni Ijumaa ya tarehe 28 Septemba, 2012 tunelekea Mbagala saa 2.30 usiku, ile tunaingia ndani dereva anatoka Kituoni Trafiki wa kike alituona akakodi Teksi akatufukuza akatupata Mivinjeni akaamuru twende moja kwa moja hadi Kilwa Road Kituo cha Polisi, ilibidi tutafute usafiri mwingine Dereva na Konda tuliwaancha LUPANGO!!!

    ReplyDelete
  3. Haya wakina mama wapika Gongo Kigogo Mbuyuni Maafande wa Kike hao wanakuja wakiwa na bunduki mikononi na Gwaride lao !...mwageni ndoo za Gongo lenu mkimbie Msituni mutafungwaaa!!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...