Habari zilizotua sasa hivi kwenye deski la Breaking Nyuzzzz la Globu ya Jamii zinasema Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya NBC Bw. Lawrence Mafuru amejea kazini baada ya kuwa nje kwa miezi kadhaa kupisha kile kilichotajwa kuwa ni uchunguzi wa masualaa kadhaa yaliyoibuka katika benki hiyo kubwa nchini. Habari za jikoni toka NBC zinathibitisha kwamba Mwenyekiti wa bodi ya Nbc Dkt Mussa Juma ameshawatangazia wafanyakazi wote kwamba Bw. Mafuru anarejea kazini kuendeleza libeneke, na kwamba alitegemewa kuanza kazi rasmi leo. Tayari taarifa kwa vyombo vya habari kuhusu habari hii imeshatolewa, na kupokelewa kwa furaha na wadau wengi.Globu ya Jamii imeshapokea taarifa hiyo na itakuwa hewani hivi punde. Habari zaidi kwa undani zitakufukia baada ya muda.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. I am soooooooooo happy! Welcome back brother Mafuru, NBC inakuhitaji sana. Wale staff wavivu na wazembe ambao bado wanadhani ukiwa staff wa benki "umeukata" na hivyo kufanya kazi kwa maringo, jasho litawatoka kwani mshua Mafuru hana masihara kwa staff kama hao. All the best.

    ReplyDelete
  2. All the Best Mr. Lawrence Mafuru !

    Ama kweli fitina ina mkono mrefu, yaani wamepenya hadi kwa Makaburu kwenye Bodi ya Utawala wakachoma, lakini Mungu Mkubwa jamaa amerudi.

    Kama ipo ipo tu, mwende mkalime mmeshindwa, mtashindana na Mungu?

    ReplyDelete
  3. Karibun Mafuru pambana na wale wano dhani NBC ni shirika la umma hivyo wanataka kufanya kazi kama wanavyo penda.Asye taka kufanya kzi kwa juhudi ajitoe mwenyewe

    ReplyDelete
  4. Hao waliopenya Kwenye Bodi ya Utawala kwa Makaburu na kumwaga fitina wametumia rushwa ya chupi ama kukaa uchi na si kinginecho!

    Kaburu hana tofauti na Mwitaliano kwa mkao wa mikasi ni mbovu sana!

    Kaburu anakosa akitegewa na wategaji?

    ReplyDelete
  5. All the best bw. Mafuru. Taasisi kubwa kama hiyo ABSA haiwezi kukurupuka kuchunguza majungu tu. Ni taasisi makini sana na shughuli zake ni njeti. Kwa mfano suala la reputation ni nyeti sana kwao. Kwa kawaida hata kama madudu yamekutwa, si kawaida kumfukuza CEO kwani hivyo kutasababisha reputation mbaya sana na pia bodi itabidi iwajibike pia. Hivyo kawaida ni kuwa hata kama madudu yamekutwa ni kawaida kumrudisha CEO alafu kumdhibiti na baadae wateja wakishatulia kufanya mabadiliko ya watendaji. jo.bura dar.

    ReplyDelete
  6. Hongera Mafuru, mwenye haki hata aibika milele. Just mapito hayo. Sasa Ma Whistle blower fanyeni kazi acheni majungu.Aibu!!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...