Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bandera , Oktoba mosi  mwaka huu alifanya ziara ya kikazi ya siku mbili katika Wilaya mpya ya Gairo. 

 Katika ziara hiyo, iliyomchukua kufika hadi Kata ya Chanjale, ambapo moja ya mambo ambayo aliyashuhudia ni suala la uharibifu mkubwa wa maliasili ya misitu kunakofanywa na baadhi ya watanzania wenye tamaa ya kuhitaji fedha za haraka. 

Hata hivyo Msitu wa hifadhi ya asili wa Kumbulu ,umeharibiwa vibaya kutokana na ukataji wa miti ovyo , uchomaji wa mkaa na upasuaji wa mbao , vitendo hivyo vikomeshwe mara m oja.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro,Joel Bendera pamoja na ujumbe wake wakiangalia lundo la Magogo yaliyokuwa yamekusanywa sehemu moja kwa ajili ya kuchomwa moto.
Askari Polisi wa Wilaya ya Gairo akifanya kazi ya kuharibu tanuli lililokuwa likichoma mkaa.
Msitu wa Hifadhi ya Asili wa Kumbulu ukiwa katika hatari ya kutokomezwa.
Wananchi wa kijiji cha Namba 30,kijiji cha Kumbulu wakimsikiliza kwa makini Mkuu wa Mkoa wa Morogoro,Joel Bendera (hayupo pichani) juu ya hali ya uharibufu wa Mazingira.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...