Habari ya asubuhi kaka Issa, 
Samahani naomba uniwekee tangazo nimedondosha wallet yangu katika basi la mwananyamala stesheni asubuhi wakati nakuja kazini.

Naomba mtu yeyote atakae ona vitambulisho vyangu tafadhari anidondoshee hapa TRA makao makuu au anipigie simu namba 0713296053  naitwa mathias Chanila. Wallet ilikuwa navitambulisho vyangu vyote

regards
Asanteni

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 17 mpaka sasa

  1. Sasa wewe Bosi Mzima na Vitambulisho nyeti kama hivyo wa Saccos kama TRA ungali unatumia usafiri mbovu wa mabasi?

    Au ndio kujificha ya kuwa wewe sio mlaji Rushwa na unapanda Mabasi?

    Au ndio ubahili uliopindukia hata kununua Vitz inakuwa ngumu?

    Inaeleweka hata Mesenja wa ndani ya Mamlaka yenye 'Ulaji' kama TRA hawezi kukosa hata uwezo wa kununua Pikipiki ya kuendea kazini!

    ReplyDelete
  2. Au ndio umekuwa Nyerere na wewe?

    Wenzio ktk TRA wanamiliki magarti huku wakiwa Vijogoo kwa kununulia magari vimada na kuwajengea majumba wewe ungali unapanda mabasi!

    Au ndio 'babu' alivyokushauri kutumia usafiri wa mabasi sio?

    ReplyDelete
  3. Ubahili mwingine jamani??

    Kwa nini ukienda kazini usikodi Teksi?

    Wewe unaingiza hela kibao pale TRA lakini bado unatumia mabasi!

    ReplyDelete
  4. Ahhh!

    Sio bure hii wewe Afisa wa Mamlaka.

    Ukizidisha kufuata mshariti sana ya Wataalamu ndio kama hapa yanakukuta sasa.

    Yaani unafanyakazi kwa miaka kibao na kuwa na cheo ktk Mamlaka kama hiyo yenye wizi na rushwa kupita maelezo halafu bado unapanda mabasi?

    Mbona wenzio kila mmoja ana usafiri wake?

    ReplyDelete
  5. Ahhh!

    Sio bure hii wewe Afisa wa Mamlaka.

    Ukizidisha kufuata mshariti sana ya Wataalamu ndio kama hapa yanakukuta sasa.

    Yaani unafanyakazi kwa miaka kibao na kuwa na cheo ktk Mamlaka kama hiyo yenye wizi na rushwa kupita maelezo halafu bado unapanda mabasi?

    Mbona wenzio kila mmoja ana usafiri wake?

    ReplyDelete
  6. Naona unataka watu wakifanyie wema wakati wewe ukiwa ofisini kwako unazingua sana watu wanaotaka huduma yako.

    Anyway watanzania wavumilivu sana watakuletea tu ofisini wallet yako. Hofu ni kwamba kabla hajakueleza amekuja kufanya nini ofisini kwako unaweza kuanza kumkoromea au kumdai rushwa wakati amekuletea waleti wako. Maana wabongo mkiwa kazini au ofisini kwenu hamjali wala kuthamini watu

    ReplyDelete
  7. Wewe Mathias Chanila au unafanya Igizo la wasifu wa Kambarage Nyerere kwenye wiki hii ya maadhimisho ya kifo chake?

    Yaani wengi hatukuelewi kabisa humu Jamvini ukiwa ni Afisa wa TRA tunayoijua ilivyokomaa kwa rushwa , wizi na ufisadi halafu wewe ukashindwa hata kuwa na Bajaj ya kuendea kazini?

    Kama ni Igizo la wasifu wa Nyerere, huna mpinzani ni wazi utakuwa umeshinda!

    ReplyDelete
  8. Afisa wa tra huyo sheikh au dakitari wako anakushauri vibaya!

    Kwa ubahili huu ulio nao kushindwa hata kukopa kazini uwe na usafiri wako ukawa unapanda mabasi.

    ReplyDelete
  9. Yaani TIN, Leseni za Magari na VAT nazotupiga hela ndefu mkiwa sambamba na wale vijana wenu vishoka umeshindwa hata kununua Toyo ama Bajaj kuwendea kazini kwako?

    ReplyDelete
  10. Bosi wa TRA,

    Yaani vishoka vyote vile mnavyotupiga unashindwa hata kukodi taksi kwendea kazini?

    ReplyDelete
  11. Bosi TRA dahhh!

    Una tambiko gumu sana la kutopanda gari la peke yako unaona sasa yamekukuta?

    ReplyDelete
  12. TRA ....na bado unapanda daladala sasa utaibiwa wewe

    ReplyDelete
  13. Bwana Mathias Chanila,
    Huyo 'Dakitari' wako mwambie akupunguzie mashariti ya kisayansi ambayo hayaendani na wakati kabisa kulingana na sehemu yako ya kazi TRA panapojulikana pana mapesa!

    Kukwambia mashariti ya kuwa daima utumie 'usafiri wa Halaiki' amekubana sana na ndio maana yote haya yanakukuta wakati uwezo unao hata kwa kukopa ukawa na gari lako badala ya kupanda mabasi!

    ReplyDelete
  14. acheni kuwafikiria wenzenu vibaya jamani. kuweeni wastarabu. mtu hamumjui. sengine mfagiaji au mtu wakawaida. WATANZANIA KUWENI WASTARABU MIWE WANGA WAMCHANA.

    ReplyDelete
  15. Ankal naomba urudishe ile article fulani aliandika mdau kuhusu tabia zetu sisi watanzania.

    Mtanzania......
    Mtanzania......
    Mtanzania.....

    David V

    ReplyDelete
  16. duh naona wabongo mna hasira na watu wa TRA. Sion hata anayempa pole huyu mtu aliyepotelewa.

    Kama kweli anafanyia TRA basi somo amelipata.

    Kwa hali hii ni dalili kuwa kuna chuki kubwa sana kati ya mwenye kazi nzuri (au mwenye nacho) na asiye na kazi nzuri/asiye na kazi kabisa(asiyenacho. Na hii hali ni hatari kwa mstakabali wa amani na taifa letu.

    ReplyDelete
  17. Nimekukubali David V, nimegundua ufisadi hauwezi isha kama kila comment inamwona jamaa wa TRA bwege kwa kukosa usafiri kumbe kila mmoja akipata madaraka atachakachua tu

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...