Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Jakaya Kikwete amemteua Prof. Mwajabu Possi (wa pili kushoto) kutoka chuo kikuu cha Dar es salaam kuwa Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) kwa kipindi cha miaka mitatu kuanzia tarehe 8 Octoba, 2012.
Kufuatia uteuzi huo, Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara amewateua wajumbe mbalimbali wa bodi hiyo ambao ni Dkt Mariam Nchimbi, Gideoni Mbalase, Prof. Elizabeth Kiondo na Balozi Kassim Mwawando.
Wajumbe wengine ni Mkurugenzi wa Idara ya Habari -MAELEZO Assah Mwambene, Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu Salva Rweyemamu, Mkurugenzi wa Idara ya Habari -MAELEZO Zanzibar Yusuf Omary Chunda pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji Tanzania Clement Mshana.
Wakati huo huo Waziri Mkangara amemteua Christopher Gachuma kuwa Mwenyekiti wa bodi ya Chuo cha Maendeleo ya Michezo Malya.
Aidha amewateua Pendo Malebeja, William Erio, Richard Ndassa, Lina Kessi, Leornard Thadeo na Allen Alex kuwa wajumbe wa bodi hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...