Profesa
Alexander Nyangero Songorwa (pichani kulia) ameteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori (Wildlife Division ) kuziba nafasi iliyokuwa wazi.
Kabla ya kuteuliwa Profesa Nyangoro alikuwa
Profesa Mshiriki katika Usimamizi wa Wanyamapori, Chuo
Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), Morogoro. Pia ndiye aliyekuwa Mkuu wa Idara hiyo ya Usimamizi wa
Wanyamapori SUA.
Wakati huohuo, Profesa Jafari Ramadhani Kidegheshon (chini)
ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Msaidizi, kuiongoza Sehemu ya Matumizi Endelevu ya
Wanyamapori (Sustainable Utilisation of
Wildlife Section). Kabla ya uteuzi huo Profesa Ramadhani alikuwa Profesa Mshiriki katika Usimamizi wa
Wanyamapori katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), Morogoro.
Uteuzi huo umetekelezwa na
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Bibi Maimuna Tarishi kwa mamlaka
aliyo nayo kwa mujibu wa kifungu cha 6 (1) (b) cha Sheria ya
Utumishi wa Umma Na. 8 ya mwaka 2002. Utekelezaji wa uteuzi huo ni kuanzia tarehe
24 Septemba 2012.
Mkurugenzi mpya wa wanyamapori, Profesa. Songorwa, ni msomi katika fani ya Wanyamapori. Anayo shahada ya
kwanza (B.Sc.) ya Sayansi katika Zoolojia na Ekolojia ya Wanyamapori ya Chuo
Kikuu cha Dar es salaam (mwaka 1987), Shahada ya uzamili (MSc) katika Mipango
na Maendeleo Vijijini ya Chuo Kikuu cha Guelph, Ontario, Canada (1994) na
shahada ya uzamivu (PhD) katika Uhifadhi Maliasili ya Chuo Kikuu cha Lincoln,
New Zealand (1999).
Kabla ya kujiunga na SUA mwaka
2001, Prof. Songorwa alikuwa mwajiriwa wa Idara ya Wanyamapori katika Wizara ya
Maliasili na Utalii kuanzia mwaka 1982.
Akiwa Wizarani Profesa Songorwa
alihudumu katka nafasi mbali mbali zikiwemo Askari Wanyamapori, Mkuu wa Kanda
na Msaidizi wa Mkuu wa Mradi katika Pori la Akiba la Selous. Pia alihudumu kama
Afisa Mwandamizi katika Mradi wa Uhifadhi Shirikishi wa Wanyamapori, Makao
Makuu, Dar es salaam.
Naye Profesa
Kideghesho siyo mgeni katika Idara ya Wanyamapori. Kabla ya kujiunga na na
SUA mwaka 1999 Prof. Kideghesho alikuwa mwalimu katika Chuo cha Usimamizi wa
Wanyamapori Mweka (CAWM-Mweka), Moshi kuanzia 1993.
Kitaaluma Prof. Kideghesho ana shahada ya
kwaza (B.Sc.) katika Kilimo ya SUA (1993), Shahada ya Uzamili (MSc) katika
Biolojia ya Uhifadhi ya Chuo Kikuu cha Kent, Uingereza (1996), na Shahada ya Uzamivu
(PhD) ya Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Norway kilichopo mjini
Trondheim (2006).
George Matiko
MSEMAJI
WIZARA
YA MALIASILI NA UTALII
22
Oktoba 2012



Hongera na Pole Mkurugenzi kazi mbele yako ni kubwa sana hasa ongezeko la vitendo vya ujangili hasa wa tembo, twiga na pundamilia. Watumishi wamekosa motisha, kwahiyo kazi kwako kuwapa ari na nguvu na waweze kujiamin ili wakusaidie vizuri. MaProfessor misisamo yenu thabiti mukiwa SUA tunaifahamu tunaamini ubabaishaji Wildlife Division sasa basi
ReplyDeleteHongereni sana walimu wangu. Nimefurahi kuteuliwa kwenu kwani wote mna uzoefu na idara ya wanyapori na maliasili kwa ujumla. Tuko pamoja nanyi.
ReplyDelete