Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akimpongeza Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa Nchini Tanzania Alberic Kacou kufuatia Umoja wa Mataifa kutimiza Miaka 67 tokea kuasisiwa kwake. Pongezi hizo amezitoa Ofisini kwake katika Ukumbi wa Baraza la Wawakilishi uliopo Mbweni nje kidogo ya Mji wa Zanzibar.
Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa aliyepo Tanzania Bw. Alberic Kacou akizungumza na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi.
Balozi Seif Ali Iddi akisalimiana na Mwakilishi Mpya wa Shirika la Mpango wa Maendeleo la Umoja wa Mataifa Zanzibar Bibi Anna Senga.Kulia ni Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa Nchini Tanzania Bwana Alberic Kacaou na kushoto kwa Balozi Seif ni Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Dr. Khalid Salum Mohd.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...