Balozi wa Kudumu wa Ubalozi wa Tanzania Katika Umoja wa Mataifa, Tuvako Manongi, akizungumza siku ya Jumatatu,wakati wa Uzinduzi wa Tathmini ya Miaka Minne ya Shughuli za Maendeleo za Umoja wa Mataifa ( QCPR). Uzinduzi ambao umefanyika wakati wa Mkutano wa Baraza la Uchumi na Fedha ( ECOSOC)la Baraza Kuu la 67 la Umoja wa Mataifa. Tanzania ni Makamu Mwenyekiti wa Baraza hilo.
Katika mchango wake Balozi aliwataka wajumbe wa mkutano huo kujadili hali halisi ya matatizo ya kiuchumi , kuongezeka kwa umaskini na upunguaji wa misaada ya kimaendeleo kwa nchi hasa zinazoendelea na nafasi ya Umoja wa Mataifa katika ufadhili na usimamiaji wa miradi ya mendeleo badala ya nchi wanachama kutumia muda mwingi kujitafutia uhalali na umaarufu. Mkutano huo ulifunguliwa na Naibu Katibu Mkuu, Bw. Jan Eliasson.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...