Balozi wa  Kudumu wa Ubalozi wa Tanzania Katika Umoja wa Mataifa, Tuvako  Manongi, akizungumza  siku ya  Jumatatu,wakati wa Uzinduzi wa Tathmini ya Miaka  Minne ya Shughuli za Maendeleo za Umoja wa Mataifa ( QCPR). Uzinduzi ambao umefanyika  wakati wa Mkutano wa Baraza la Uchumi na Fedha  ( ECOSOC)la Baraza Kuu la 67 la  Umoja wa Mataifa. Tanzania ni Makamu Mwenyekiti wa  Baraza hilo.   
Katika mchango wake Balozi aliwataka wajumbe wa mkutano huo kujadili hali halisi ya  matatizo ya kiuchumi , kuongezeka kwa umaskini na upunguaji wa misaada ya  kimaendeleo  kwa nchi  hasa  zinazoendelea na  nafasi ya  Umoja wa Mataifa katika  ufadhili na usimamiaji wa miradi ya mendeleo  badala ya nchi wanachama kutumia muda mwingi kujitafutia uhalali na umaarufu. Mkutano huo ulifunguliwa na Naibu Katibu  Mkuu, Bw. Jan Eliasson.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...