Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein akifurahia jambo na Meneja Mahusiano ya Nje wa Vodacom Bw Salum Mwalim mara baada ya kupokea hundi yenye thamani ya shilingi Milioni Kumi na Tano mchango wa Vodacom Foundation kwenye mfuko wa maendeleo ya watu wenye ulemavu Zanzibar. Wa kwanza kushoto ni Mkuu wa Idara ya Mahusiano na Mawasiliano wa Vodacom Bi Joseline Kamuhanda. Vodacom ilikabidhi hundi hiyo katika hafla ya uzinduzi wa mfuko huo iliyofanyika mwishoni mwa wiki Mjini Zanzibar.
 Mkuu wa Idara ya Mahusiano na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania Bi Joseline Kamuhanda.akitoa salaam za Vodacom Tanzania wakati wa hafla ya chakula cha usiku iliyoandaliwa na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar kuchangia mfuko mpya wa maendeleo ya watu wenye ulemavu Zanzibar iliyofanyika mwishoni mwa wiki mjini Zanzibar. Vodacom Tanzania ilichangia Shilingi Milioni Kumi na Tano kupitia mfuko wake wa kusaidia jamii - Vodacom Foundation.
 Wafanyakazi wa Vodacom Tanzania kutoka kushoto Meneja Mahusiano ya Nje Bw. Salum Mwalim, Mkuu wa Idara ya Mahusiano na Mawasiliano Bi. Joseline Kamuhanda na Meneja Kanda ya Zanzibar Bw. Mohamed Mansour wakipokea utambulisho wa kuwa miongoni mwa wadhamini wakuu waanzilishi wa mfuko wa Manedeleo ya watu wenye ulemavu Zanzibar wakati wa hafla ya uzinduzi wa mfuko huo iliyofanyika mwishoni mwa wiki Zanzibar. Wa kwanza kulia ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo wa Zanzibar Mh. Said Ali Mbarouk.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein akihutubia wadau mbalimbali waliohudhuria hafla ya chakula cha jioni  iliyolenga kuuzindua rasmi mfuko wa maendeleo ya watu wenye ulemavu Zanzibar mwishoni mwa wiki mjini Zanzibar. Wa kwanza kushoto ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad. Hafla hiyo iliandaliwa na Ofisi ya Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar Vodacom Tanzania ilichangia Shilingi Milioni Kumi na Tano kupitia mfuko wake wa kusaidia jamii - Vodacom Foundation.
Kwa habari kamili BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...