Mkurugenzi Mwendeshaji wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi za Jamii (NSSF),Cricentus Magori akipigia kura Maajabu saba ya Afrika katika moja ya kituo cha kupigia kura hizo kilichokuwepo katika Hoteli ya Naura Springs,jijini Arusha hivi karibuni. Vivutio hivyo ni Mlima Kilimanjaro, Hifadhi za Wanyama za Serengeti na Ngorongoro. Zoezi hili linafanywa na wakala wa TANAPA kushirikiana na wadau mbalimbali ili kufanikisha ushindi wa Tanzania.Kulia ni Mratibu wa Zoezi la upigaji kura wa Maajabu saba ya Afrika, Herman Minja.
Mratibu wa Zoezi la upigaji kura wa Maajabu saba ya Afrika, Herman Minja (katikati) akimpatia maelekezo kwa Afisa Utamaduni wa jiji la Arusha ya namna ya upigaji kura wa vivutio vya nchi yetu kwenye Shindano la Maajabu Saba ya Afrika.Kulia ni Mdau Mroki Mroki wa Father Kidevu Blog nae akipigia kura Maajabu Saba ya Afrika.




Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...