Rais wa Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji wa Kimbari ya Rwanda (ICTR) Vagn Joensen akiwasilisha taarifa yake ya mwaka mbele ya Baraza Kuu la 67 la Umoja wa Mataifa mwanzoni mwa wiki, katika taarifa yake hiyo ambayo alisema ni ya mwisho kwake kama Rais wa ICTR ambayo iko ukingoni mwa kukamilisha majukumu yake pamoja na ile ya iliyokuwa Yugoslavia ya Zamani (ICTY) iliyowasilishwa na Rais wake Theodor Meron. Alieleza bayana kwamba baadhi ya changamoto zilizo mbele ya Mahakama hiyo ni Nchi za kuwahamishia watu ambao ama wameachiwa huru na Mahakama hiyo na au wamemaliza vifungo vyao. Watu hao ambao wanakadiriwa kuwa nane wanaendelea kuhifadhiwa katika nyumba salama ( Sefu House) Jijini Arusha Nchi Tanzania.
Balozi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Tuvako Manongi akizungumza wakati wa upokeaji wa taarifa za mwaka za mahakama za kimataifa za ICTR na ICTY. Pamoja na Mambo mengine, Balozi Manongi alisizihisi nchi wanachama wanachama wa Umoja wa Mataifa kulipokea ombi la Mahakama ya ICTR kwa mtizamo chanya hususani kwa kutoa ushirikiano wa kuwapokea watu hao ambao wanahitaji nchi za kwenda. Akasema suala hilo ni nyeti na ni la haraka hasa kwa kuzingatia kuwa mahakama hiyo inamaliza muda wake. Kama watu hao watakosa mahali pakwenda kuna hatari ya kuendelea kuhifadhiwa nchini Tanzania. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...