·        Eneo la Polisi Oysterbay halijauzwa na haliuzwi.
·        Eneo linalohusika sio Bwalo la Polisi bali Polisi Oysterbay.

·        Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi imetafuta mwekezaji kwa lengo la kuwekeza katika eneo la Polisi Oysterbay lenye ukubwa wa ekari  24. Uwekezaji huo utawezesha kujengwa kwa nyumba za makazi 350 ya Polisi katika maeneo ya Mikocheni na Kunduchi jijini Dar es Salaam na Kituo cha Polisi cha kisasa katika eneo hilo la Oysterbay.
·        Mshauri Mwelekezi wa Mradi huo ni Bureau for Industrial Cooperation (BICO) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
·        Mwekezaji aliyepatikana baada ya kufuata taratibu zote za Manunuzi ya Serikali kufanyika ni Mara Group Ltd. ya nchini Uganda.
·        Tenda ilitangazwa kimataifa.
·        Kampuni 10 zilishiriki katika tenda hiyo.
·        Mkataba wa Awali kati ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi na Mwekezaji huyo umesainiwa tarehe 23 Juni, 2012.
·        Gharama za uwekezaji katika eneo hilo ni karibu shilingi 426.6 bilioni.
·        Kufuatana na Mkataba wa Awali, Mwekezaji huyo atajenga nyumba za makazi 350 kwa ajili ya Jeshi la Polisi jijini Dar es Salaam na Kituo kipya cha kisasa cha Polisi katika eneo hilo, kwa gharama ya shilingi 31.6 bilioni.  Fedha hizi zitalipwa kutokana na tozo atakalokuwa analipa Mwekezaji.
·        Kufuatana na Mkataba wa Awali, Mwekezaji atalipa tozo la shilingi 4.36 bilioni kila mwaka kama malipo ya matumizi ya ardhi na majengo na tozo hili litakuwa linapanda kufuatana na mwenendo wa uchumi wa nchi.
·        Kufuatana na Mkataba, ardhi na majengo yote atakayojenga Mwekezaji yatabaki kuwa ni mali ya Serikali na  yeye atakuwa mpangaji tu.
·        Mwekezaji atajenga Maduka makubwa (Shopping Malls), Hospitali kubwa ya kisasa, Ukumbi wa Mikutano, Hoteli ya kisasa, Ofisi za kukodisha, Makazi ya kukodisha na Maeneo ya maegesho ya magari.
·        Mradi utanarajiwa kuanza mwezi Julai, 2013 baada ya kusaini Mkataba.
·        Mkataba wa Mradi ni wa miaka 50.
(Unaweza pia kutembelea Tovuti ya Wizara, www.moha.go.tz kupata taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari tarehe 14 Novemba, 2012).

Imeandaliwa na Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 8 mpaka sasa

  1. Good idea BUT....!!!

    Hii mikataba ya miaka 50, shuti WADANGANYIKA TUWE MACHOOOOO...! Inatakiwa huu uwekezaji uangaliwe kwa jicho l;a 3,4.. Hapo milimani kumewekweza majengo ambayo YANA NYUFA BALAA, hata miaka 50 sidhani kama yatafika. Kama tunataka majengo ambayo mwekezaji anatuachia ni budi kuwe na usimamizi wa kutosha wa kuzingatia QUALITY. Wasiachwe wenyewe,

    ReplyDelete
  2. Yaani POLISI wetu wakakae mbali Kunduchi Mtongani, je wakihitajika maeneo ya Oysterbay, Msasani, Ada Estate, Mwananyamala n.k watafikaje haraka? au Kampuni za ulinzi za binafsi ndiyo watatoa huduma hiyo ya usalama kwa raia?

    Hii kitu inaitwa OPEN GOVT au UWAZI WA SERIKALI, kwa nini hawakushirikisha umma au jamii kabla ya kusaini mkataba wa mradi maana na sisi wadau kupitia POLISI JAMII tungetoa maoni yetu.
    Mdau
    Maeneo Morocco DSM

    ReplyDelete

  3. Hii haijakaa vizuri, jeshi la polisi linategemea mwekezaji!!!
    Kama hakuna uwezo acheni kwanza, hakuna ulazima wowote wa kutuwekea "Kituo cha polisi cha kisasa" ili iweje? Ki ostabei polisi chetu kiacheni hivyo hivyo maana tunakataa utata.

    Mwisho mtapata na sababu za kuleta mwekezaji Lugalo na Mgulani.

    ReplyDelete
  4. Huu uwekezaji sio mzuri kwani muwekezaji amewekeza asilimia 7.4 kwa walengwa kwenye jumla ya pesa yote ambayo anakuja kuwekeza maana jumla ni billion 426.6 angalieni wenyewe ni billion 31.6. Hawa jamaa wamebenefit sana maana faida watakayoipata kwa huu mradi ni kubwa ndio maana nimeangalia website yao wana offer 22% kama faida kwa mwaka kwa watu watakao invest kwenye kampuni ya hawa jamaa ni ma middle man au kitaalamu ni intermediary. Kweli watanzania bado tumelala ningependa kujua kama huu mradi ni mmoja ya miradi ya serikali iliyo kwenye PPP na kama ni hupo huko naomba serikali ijaribu kuwaelimisha Watanzania juu ya PPP ili wazawa waweze kufaidika zaidi.
    Mdau UK

    ReplyDelete
  5. badala ya kushughulika na ulinzi wako kwenye kukimbizana na wawekezaji.

    ReplyDelete
  6. Pamoja na maelezo marefu mimi nakataa huu uwekezaji. Kwani serikali inashindwa vipi kujenga kituo cha kisasa cha Polisi? Kodi zetu zinakwenda wapi? Hao wawekezaji ndio watakaokuja kuitia mfukoni serikali kwa kupistisha mali zao bila ushuru wala kodi kisa wameisaidia serikali kijengea miundombinu. Maajabu haya yanatokea Tanzania tu, kila kukicha wawekezaji wawekezaji wawekezaji.....

    ReplyDelete
  7. Tanzania sasa hivi kuna sheria ya PPP (PPP Act 2010). Kwa bahati mbaya sidhani kuwa sheria hii imefuatwa hivyo kwa maana nyingine WIZARA IMEVUNJA SHERIA.

    ReplyDelete
  8. Jamani tunaelekea wapi sasa?

    Hivi Mamlaka kama Polisi au Wizara ya Mambo ya Ndani na masuala ya uwekezaji wapi na wapi?

    Hivi kweli ni busara kuiruhusu Wizara na Idara ya Polisi kuingia Mikataba ya Kibiashara na uwekezaji badala ya ''kusimamia jukumu lao la Kiapo'' la ''Usalama wa Raia na mali zao''?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...