Mhe. Tuvako Manongi, Balozi wa Kudumu wa Ubalozi wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa,  akizungumza wakati Baraza Kuu la 67 la Umoja wa Mataifa  lilipokutana mwishoni mwa wiki kujadili  taarifa ya mwaka ya kazi za Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa, na pia kujadili kuhusu ajenda ya  kulifanyika mageuzi ya kimfumo ya Baraza hilo kwa kuongeza nafasi za uwakilishi wa kudumu na  nafasi zisizo za kudumu. Majadiliano ya kulifanyika mageuzi  Baraza hilo yameshadumu kwa zaidi ya miaka 20 sasa na mpaka sasa hakuna dalili zinazoonyesha kwamba mabadiliko yanaweza kutokea mapema iwezekanavyo. Afrika inadai viti  viwili vya kudumu   vikiwa na haki ya kupiga kura ya vito na pia inataka viti vitano visivyo vya kudumu kwa mujibu wa  Makubaliano ya Ezulwini

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa


  1. Ukoloni mamboleo at its peak.

    Maslahi (Nishati na Madini) na ubabe (Kutawala Dunia) ndiyo vinapelekea Afrika na wenzetu wengine kubinywa.

    Watetezi wetu hapo ni warusi na wachina. Wao hawana ndoto za kutawala Dunia.

    ReplyDelete
  2. We Anonymous wa Sat Nov 17, 12:20:00 PM 2012;
    Unasema nini? Warusi na Wachina hawana ndoto za kututawala?! Huoni wamejaa kibao bongo na misaada yao? Na wachina ndio kabisa wanakimbiza Africa. Yaani hapo hamna kuchagua wote ni mashetani, chaguo lako tu, wote wabaya.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...