WAANDISHI WA HABARI MKOA WA MOROGORO NA TASNIA NZIMA YA HABARI NCHINI WAMEPATWA NA MSIBA MKUBWA KUFUATIA KIFO CHA GWIJI WA HABARI NCHINI, MPIGANAJI AIDAN LIBENANGA, ALIYEFARIKI GHAFLA SAA 12 : 15 ASUBUHI YA NOVEMBA 18, MWAKA HUU. 

KWA MUJIBU WA NDUGU NA WATOTO WA MAREHEMU, MAZISHI YANATARAJIWA KUFANYIKA NOVEMBA 20, MWAKA HUU( JUMANNE ) MJINI MOROGORO. BAADHI NI PICHA ZA NDUGU NA MAJIRANI HUSUSANI WAANDISHI WA MOROGORO WAKIWA NYUMBANI KWA MAREHEMU MTAA WA SABASABA. 

MAREHEMU ALIKUWA MMOJA WA WAANDISHI WA HABARI WAKONGWE ALIYEWAHI KULITUMIKIA SHIRIKA LA HABARI TANZANIA ( SHIHATA) ENZI HIZO . 

 Mungu ailaze pema peponi roho ya marehemu 'Libes' Picha na maelezo na John Nditi.
Hayati Aidan Libenanga
Akina mama wakimfariji mtoto wakike wa Marehemu Aidan Libenanga
Baadhi ya waandishi wa habari wakiwa nyumbani kwa marehemu Aidan Libenanga , eneo la Sabasaba, Mjini Morogoro, akiwasiliana na jamaa zao na kumsikiliza mwanae Rama.
Mtoto wa kwanza wa kiume wa Hassan Libenanga ( kulia) akifarijiwa na kijana mkazi wa Sabasaba 
Ramadhan Libenanga (kushoto) mtoto wa marehemu akizungumza na Meya wa Manispaa ya Morogoro, Mstahiki Amiri Nondo, nyumbani kwa marehemu 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. poleni sana kwa msiba wanafamilia mungu ailaze mahala pema peponi roho ya marehemu.najua mko ktk kipindi kigumu ila mungu atawawezesha kuwa na subira.inshallah.mzee wetu alikua kiungo mji kasoro ila mola ndiye ajuae.inna lillahi wa inna lillahi rajiuni.
    mayor M.

    ReplyDelete
  2. Poleni sana kina Kuti. Mungu awape nguvu katika kipindi hiki kigumu.

    ReplyDelete
  3. Poleni sana akina Kuti na Bossnoja

    ReplyDelete
  4. Rambirambi kwa famili.Poleni.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...