MILIONI sita zinahitajika kwa ajili ya matibabu ya mtoto Selemani Said (1), ambaye anajisaidia haja kubwa kupitia utumbo mkubwa huku ukiwa nje ya tumbo lake imeleezwa.
Akizungumza na wandishi wa habari Katika Ukumbi wa Idara ya Habari (Maelezo),jijini Dar es Salaam leo, mama wa mtoto huyo, Veronika Laurent ambaye ni Mkazi wa Bunju, alisema mtoto huyo alizaliwa huku akiwa na sehemu ya kutolea haja kubwa lakini cha kushangaza, haja kubwa ilikuwa ikitokea mdomoni.
Alisema msaada wa fedha hizo utasaidia katika kumfanyia operesheni mtoto huyo ambaye kwa sasa anaishi akiwa katika mateso makubwa.
Veronika alisema hivi sasa yeye pamoja na mwanaye huyo wanaishi maisha ya kubahatisha baada ya baba wa mtotohuyo kuitelekeza familia hiyo kutokana na hali ya ugonjwa wa mtoto huyo.
“Mimi ni nachoomba ni msaada wa fedha ili niweze kumpeleka kwenye matibabu kwani sina msaada wowote,ukichukulia wazazi wangu kufariki na hivi sasa naishi kwenye nyumba ya mwenyekiti wa Mtaa wa Bunju wilayani Kinondoni jijini baada ya kushindwa kupangisha chumba kwani sina kazi yeyote”alisema.
Aidha, alisema hadi utumbo wa mtoto huyo kutoka nje, ni baada ya kufanyiwa operesheni katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili ambapo hata alipompeleka tena kwa ajili ya matibabu alikosa ushirikiano kutoka kwa madaktari na wahudumu wengine.
Alisema kwa yeyote ambaye yuko tayari kumsaidia anaweza wasiliana naye kwa kupiga simu namba o715 83 77 00, na namba ya mwenyekiti huyo wa mtaa 0656780236.
Veronika ni mzaliwa wa Mkoa wa Kilimanjaro eneo la Kijiji cha Uru,Moshi ambye alimzaa mtoto huyo na mwanamme aliyemtaja kwa jina la Abdalah Said, kabilake makonde mfanyabiashara wa viatu Ubungo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 10 mpaka sasa

  1. ALLAH AKBAR... UNCLE KAMA UNAWEZA TUTAFTIE M-PESA YA HUYO DADA TUMSAIDIE CHOCHOTE. SHUKRAN KWA TAARIFA.

    ReplyDelete
  2. Jamani kuna madakari wengi tangia mkunga, madaktari wa muhimbili ambao wamemuona mtoto huyo na matatizo yake lakini hakuna hata mmoja aliyeguswa na kujitolea kumsaidia mtoto huyu mapema hadi amekuwa mkubwa. Pia hospitali kubwa ya muhimbili imekataa kumsaidia mtoto huyu, jamani tunaenda wapi? Mama kapige kambi Getini wizara ya Afya. alexbura dar

    ReplyDelete
  3. Anony 06.49.00. Asante kwa maoni yako. Hata akienda hapo Wizara ya Afya unadhani watafanya kitu? Sanasana watampeleka Muhimbili halafu ataanza kupigwa tarehe za njoo baada ya wiki, kisha mwezi haya mwaka mwingine tena. Hii Wizara ya Afya inatengewa pesa nyingi sana hata sijui VIPAUMBELE VYAO NI VIPI? Sijui kama huwa wana issue za haraka kweli!!! Niliwahi kuona mtoto wa namna hii na wazazi wake walikuwa hawana uwezo kutokea Zanzibar (akigharamiwa na Serikari ya Mapinduzi) alikuja hosp. binafsi hapa Dar kwa ajili ya operesheni hiyo na ilifanikiwa. Si kwamba Muhimbili hawawezi lah! Walipeni vizuri hao jamani na vifaa wanaweza, SIO KILA KITU INDIA!!! Mbona kwenye Hospitali binafsi wanazifanya???

    ReplyDelete
  4. Pole sana mama, natumai utapata msaada lakini kwa ushauri wa haraka haraka nimepata kuona Mcungaji Kakobe akidai kuponyesha, je ummemjaribu? Hata mchungaji Lusekelo pia anaponyesha, natumai watasikia kilio chako, hata kama wao hawaingii kwenye mablog nina uhakika kuna waumini wao watafikisha kilio chako, pole sana.

    ReplyDelete
  5. Baba yake kama yupo kwanini asimshughulikie au mmetengana?Jamani mtoto anateseka sana huyo.Nitampigia huyu mama anieleze vizuri zaidi.

    ReplyDelete
  6. Siyo kwamba wamekataa kumsaidia, pengine HAWAWEZI KUMSAIDIA, in that case wampeleke India kama wanavyojipeleka wao na familia zao.

    ReplyDelete
  7. EEEE bwana eehhhh!Inshallahh ,haujazaliwa haujafa na haujafa haujazaliwa.Yaani bongo madaktari kibao ,hospital kibao na matajiri kibao ,jamani huyu mtoto kwa kweli watu kibao ni matajiri wanashindwa kumsaidia?Basi serkali iingilie kati ,fedha kibao za walipa kodi na misaada inayotolewa kwa ajili ya watoto walioko ktk mazingira magumu.Gazeti la mwananchi limeandika hivi karibuni Tanzania ni nchi ya kwanza duniani inayoongoza kwa kupatiwa misaada na mataifa matajiri,je misaada hiyo inaishia wapi?Walengwa wa misaada hiyo ni kama huyu mtoto au?UNICEF ,etc mko wapi?Matajiri mlioficha fedha uswis je mnamuona huyu mtoto?Bro michuzi fanya mpango mtoto huyu aonyeshwe hata kwenye TV live ili watu wenye uwezo wamchangie.Yaani akina Lowasa wakiumwa kichwa tuu wanaruka ughaibuni kutibiwa na wengineo kibao,je vipi huyu dogo?Madaktari Muhimbili etc muwe na utu sio kuangalia sana fedha ,huyu dogo tatizo alilonalo mnaweza kumtibu hapo bongo na mimi naongea kama mtu mwenye ujuzi kidogo na ninajua anaweza kuwekewa anuspreta na akatibiwa ,ni simple mtu kama ni mtaalamu na wataalamu tunao hapo bongo.Dogo na mama yako nawaombea kila la heri ,hatimaye msaada utaupata.Mdau

    ReplyDelete
  8. eee mungu...

    ReplyDelete
  9. Dont make excuse ya nani asaidie. Mimi na wewe tusaidie acheni maelezo ya kusukumia na kulaumu wengine. Upendo wako ni muhimu kuliko madaktari, wizara, matajiri, mawaziri nk. Do something now na stop yawning.
    Binasfi nitasaidia. Nawewe saidia. Stop pointing fingers

    ReplyDelete
  10. anonymous 05:43:00 uko sahihi kabisa. Tuchange ili mtoto apone. tuache kulalmika kuwa hao wengine wanapesa. watu wa kipato cha chini/kati 300 wakichanga kila mmoja 20,000 tunaweza kumponya mtoto huyu na tunaweza. Hima tumchangie mtoto huyu. Mimi kesho natoa mchango wangu. Mungu msaidie mtoto huyu apate matibabu. Tungependa tuje tupate feedback ya afya yake.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...