Mwenyekiti mstaafu wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Kanali mstaafu Idd Kipingu akimkabidhi nahodha wa timu ya Azam FC, Abdul Mgaya kombe la Ubingwa wa  michuano ya Uhai Cup 2012 baada ya timu hiyo kuifunga Coastal Union ya Tanga kwa penalti 3-1 katika mchezo wa fainali ya vijana chini ya miaka 20 uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam. Katikati ni Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Leodgar Tenga. 
 Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Angetile Osiah akimkabidhi zawadi ya mfungaji bora wa mashindano ya vijana chini ya miaka 20 ya Uhai Cup, Ramadhani Mkipalamoto wakati wa fainali ya michuano hiyo iliyofanyika kwenye Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam.
 Wachezaji wa Azam FC wakishangilia baada ya kukabidhiwa kombe lao.
 Golikipa wa Azam FC, Aishi Salum akiokoa moja ya hatari zilizoelekezwa langoni mwake.
Mshambuliaji wa Coastal Union, Twaha Shekue akitafuta mbinu za kumtoka beki wa Azam FC, Samwel Mkomola. Picha na Francis Dande

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...