Rais
Jakaya Mrisho Kikwete ameambiwa juzi, Jumatano, Desemba 5, 2012, kuwa ujenzi wa
Barabara ya Dar es Salaam-Lindi utakamilika katika miezi sita ijayo kuanzia
sasa.
Rais Kikwete alipewa maelezo
hayo na Naibu Waziri wa Ujenzi, Mheshimiwa Mhandisi Gerson Hosea Malangalila
Lwenge wakati aliposimama kukagua maendeleo ya ujenzi kwa akiwango cha lami wa
kilomita 56 kati ya Nyamwage, Mkoa wa
Pwani na Somanga, Mkoa wa Lindi.
Rais Kikwete alisimama
kukagua ujenzi wa Barabara hiyo wakati akirejea Dar es Salaam kutoka Lindi
ambako alifanya ziara yenye mafanikio makubwa ya siku tatu kukagua na kuzindua
miradi ya maendeleo na kusikiliza changamoto za wananchi.
Akipewa maelezo ya ujenzi wa
Barabara hiyo kwenye eneo la Somanga, Rais Kikwete aliambiwa kuwa kati ya
kilomita hizo 56 tayari kilomita 30 zimeshatiwa lami. Barabara hiyo inajengwa
na Kampuni ya MS Karafi.
Naibu Waziri huyo alimwambia
Rais Kikwete: “Mjenzi anajenga kiasi cha mita 250 kila siku na kama hapakuwepo na
kuharibika kwa lolote ama mvua isipokuwa nyingi kupita kiasi, basi ujenzi wa
Barabara hii utakuwa umekamilika katika miezi sita ijayo kuanzia sasa.”
Naibu Waziri alimwambia Rais
Kikwete kuwa ni kweli ulikuwepo ucheleweshaji kwa upande wa mjenzi, lakini sasa
maendeleo ni mazuri. Barabara hiyo ilipangwa kukamilika Juni, mwaka jana, 2011.
“Kwa jumla ujenzi wa Barabara
nzima umekamilika kwa asilimia 78, njia ya awali ambako lami itawekwa
imekamilika kwa asilimia 98, madaraja madogo kiasi cha 55 tayari yamejengwa na
vifaa vyote ikiwa ni pamoja na kokoto viko kwenye eneo la ujenzi.”
Barabara ya Dar es
Salaam-Lindi ina urefu wa jumla ya kilomita 452 na kukamilika kwa kipande cha
Nyamwage-Somanga una maana kuwa mtu yoyote anaweza kusafiri kwa lami tupu
kutoka Mtwara hadi Kagera ama Mwanza ama Arusha ama Tunduma.
Imetolewa na:
Kurugenzi
ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar
es Salaam.
07
Desemba, 2012
wakati umefika sasa hichi kipande kiishe, miaka nenda rudi mnatuambia kitaisha kitaisha. june 20013 ikifika mtatuambia june 2014 aaargh...inakera sana, wakati wa masika hapo tunalala sana.
ReplyDeletektk aya ya mwisho imesomeka kuwa ".....mtu yoyote anaweza kusafiri kwa lami tupu......."
ReplyDeletemimi ningependa isomeke angalau ....."mtu yeyote anaweza kusafiri kupitia barabara ya lami tupu......."
jamani tujitahidi kutumia kiswahili chetu vizuri..Tanzania inasemekana ndio mwasisi wa kiswahili na mimi nakubaliana na hilo hivyo tuwe mfano kweli hususan kwa idara nyeti kama KURUGENZI YA MAWASILIANO IKULU