Huduma ya M-Pesa
ilipata hitilafu jana…Wahandisi wa mtandao Tanzania wakishirikiaana na wadau wa
nchini Uingereza walifanya kazi usiku na mchana ili kutatua tatizo na hatimaye
kuwezesha huduma kufanya kazi mida ya jioni.
Mkurugenzi wa kitengo cha M-Pesa, Jacques Voogt amesema wateja walikua wakipiga *150*00#
wanapata ujumbe mfupi SMS usemao
“Ndugu mteja, huduma ya M-Pesa haipatikani kwa sasa, tafadhali jaribu tena”
Tunaomba radhi
kwa usumbufu wowote uliojitokeza kwa wateja wetu, mawakala wa M-pesa na wadau
wetu wote kwa ujumla.
M-Pesa ni huduma
pendelevu ya malipo kwa wateja zaidi ya milioni 4.5 na ina wadau wa biashara
zaidi ya 200 wanaotumia huduma hii kukusanya na kusambaza pesa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...